STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Mashetani Wekundu kumbe hawatanii kwa Griezmann

WAMEPANIA aisee! Klabu ya Manchester United inadaiwa imeanza kufanya mazungumzo ya kumuwania straika wa kimataifa wa Ufaransa, Antoine Griezmann, huku ikielezwa kuwa inatarajiwa kumpa ya mshahara wa pauni 220,000 kwa wiki ili kumshawishi kutua Old Trafford.
Duru za michezo zinadai kuwa, Mashetani Wekundu tayari wameanza mazungumzo na wawakilishi wa nyota huyo wa Atletico Madrid na imeahidi mshahara wake utafikia ule anaolipwa kiungo Paul Pogba aliyepo ndani ya klabu hiyo ya EPL.
Griezmann ameshawahi akikaririwa akieleza jinsi anavyoihusudu United na Mourinho katika mahojiano yake huko nyuma. Kama wakifikia makubaliano hayo United inadaiwa italazimika kutoa kitita cha pauni milioni 86 ili kutengua kitenzi katika mkataba wa mshambuliaji huyo ambaye amekuwa akizitoa udenda klabu nyingi barani Ulaya kwa soka lake murua.

No comments:

Post a Comment