STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 28, 2014

Golden Bush kupeleka makali yao Kilombero

Kikosi cha Golden Bush
Makocha wa Golden Bush, Madaraka Seleman na Herry Morris waliosimama wakiteta na wachezaji wao katika moja ya mechi zao
 MABINGWA wa kandanda wa soka la maveterani, Golden Bush Veterani inatarajiwa kupeleka makali yake wilaya ya Kilombero Morogoro kumenyana na Kilombero Veterani katika mechi inayochezwa kesho.
Kwa mujibu wa Msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' kikosi cha Golden Bush kitaondoka kesho asubuhi kikiwa na wachezaji 25 wakiongozwa na mkuu wa msafara,  Waziri Mahadh 'Mandieta'.
Ticotico alisema kikosi chao kitashuka dimbani jioni ya kesho kwenye uwanja wa Ruaha kuumana na wenyeji wao watakaokuwa wakiongozwa na nahodha wa zamani wa Simba, Mustafa Hozza.
Ticotico alitamba kuwa wanaenda Kilombero kuendeleza ubabe wao ambao umewafanya kukimbiwa na wapinzani na kwamba wenyeji wao wajiandae kwa kipigo.
Alisema kikosi chao chini ya kocha Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' kitaongozwa na nahodha wao Wisdom Ndhlovu a.k.a Mwakalinga.

No comments:

Post a Comment