STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 28, 2014

Subira ya Shaa mwezi ujao

Shaa katika pozi
'AUDIO' na VIDEO ya wimbo mpya wa msanii, Sarah Kais 'Shaa' unaofahamika kama 'Subira' unatarajiwa kuachiwa rasmi mapema mwezi ujao.
Wimbo huo uliobadilishwa jina kutoka 'Sifa Ujinga' hadi kuwa 'Subira' ni kazi ya pili ya mshindi huyo wa zamani wa Coca Cola Pop Star chini ya familia ya Mkubwa na wanae inayongozwa na Said Fella.
Akizungumza na MICHARAZO, Fella alisema wamepanga kutoa 'audio' na video ya wimbo huo mwezi ujao baada ya kurekodiwa mapema tangu Februari mwaka huu.
Fella alisema waliamua kuuzuia wimbo huo kutoka mapema ili kutoa nafasi ya kazi ya msanii huu iitwayo 'Sugua Gaga' kuendelea kutamba kwenye soko la muziki kutokana na ukali wake.
"Kazi mpya ya Shaa tutaiachia rasmi mapema mwezi ujao ikiwa ni 'audio' na video yake, hivyo mashabiki wajiandae kupata uhondo," alisema Fella waliyeingia mkataba na Shaa kwa muda wa miezi sita.
Kabla ya kutua Mkubwa na Wanae, Shaa alikuwa akifanya kazi chini ya umeneja wa Master J.

No comments:

Post a Comment