STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 28, 2014

Mashali, Kaseba kupima uzito leo

Kaseba na Mashali wakishoo
MABONDIA Japhet Kaseba na Thomas Mashali na wengine watakaowasindikiza katika pambano lao la kuwania ubingwa wa UBO Afrika wanatarajiwa kupima uzito wao siku ya Ijumaa jijini Dar.
Kwa mujibu wa taarifa ya mmoja wa waratibu wa pambano hilo, Ibrahim Kamwe mabondia hao watapima uzito kuanzia saa 3 asubuhi kwenye ukumbi wa hoteli ya National iliyopo eneo la Keko.
Mbali na Mashali na Kaseba watakaopambana katika pambano la raundi 10 uzito wa LightHeavy (kilo 79), pia mabondia wengine watakaopima uzito na afya zao ni Allan Kamote ambaye atapigana na Karage Suba katika pambano la kuwania taji la kimataifa ya UBO.
"Mabondia wote wameshataarifiwa na wanatakiwa kuwahi mapema siku ya Ijumaa, National Hotel ili kupima afya na uzito wao kabla ya Jumamosi kuonyeshana kazi kwenye ukumbi wa PTA," alisema.
Kamwe aliwataja wengine watakaochuana katika michezo hiyo iliyoandaliwa na promota Ally Mwazoa, ni pamoja na Fredy Sayuni dhidi ya Rajab Mahoja watakaowania ubingwa wa taifa wa PST.
Baina Mazola atacheza na Bakari Dunda,Issa Omar ataonyeshana kazi na Zuberi Kitandula, Juma Fundidhidi ya Haji Juma, Shabaan Mtengela vs Jumanne Mohamed, Jocky Hamis dhidi ya Said Chaku

No comments:

Post a Comment