STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 26, 2015

Simba waiwahi TFF kuhusu makocha wa makipa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-ErV4LDze29At9zLOJ5-K7zmESxzpny61EoTZ3Oj0BwcGnaHSSYJesvEuGbG8W3_LmcXp-5IKsJPPyMBUZZ6N0_rCe840K_0q4lFxI8OEaEgFOGs4iLDRaMuGeQX20S4EGDP4_CFZ-_A/s1600/Simba+logo+white.jpg
SIMBA wajanja sana, wakati Shirikisho la Mpira wa Mpira wa Miguu nchini (TFF) likitoa agizo na kuvioomba klabu zote zinavyoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom kuwasilisha jina la kocha wa magolikipa kufikia jumatatu ya tarehe 29 Juni, 2015 katika ofisi za TFF, tayari klabu hiyo imeshamleta kocha wake kutoka Kenya, Abdul Salim.
TFF imeandaa kozi ya magolikipa hivyo inahitaji kupata jina la kila kocha wa magolikipa ili kuweza kushiriki kwenye kozi hiyo itakayoanza tarehe 13 - 17 Julai, 2015 jijini Dar es Salaam kwa mpango huo Simba itakuwa imeikatia denge TFF mapema. Coastal Union nayo ilifanya yao mapema juzi baada ya kumsainisha kocha wa zamani wa KCC ya Uganda, Lumu Fred ili kuwanoa makipa wa timu hiyo itakayokuwa chini ya Kocha Mkuu, Jackson Mayanja pia wa Uganda aliyekuwa akiinoa Kagera Sugar katika msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment