STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 4, 2014

Barcelona wamruhusu Xavi kuhama

KLABU ya Barcelona kupitia Rais wake, Josep Maria Bartomeu imesema ipo tayari kumsaidia Xavi Hernandez kuondoka kama atataka kuihama klabu hiyo.
Nyota huyo wa timu ya taifa ya Hispania amekuwa gwiji tangu alipoanza kuichezea klabu hiyo mwaka 1998, lakini veterani huyo mwenye umri wa miaka 34 alijikuta akikosa nafasi ya kutosha katika kikosi cha kwanza chini ya kocha Gerardo Martino msimu uliopita.
Aliachwa pia nje ya kikosi cha kwanza kilichocheza mechi ya kuamua bingwa wa La Liga dhidi ya Atletico Madrid, ambayo kama Wacatalunya hao wangeshinda wangetwaa ubingwa.
Tangu wakati huo amehusishwa na klabu kadhaa, ikiwamo ya Al-Arabi ya Qatar, na bosi huyo wa Barca amemfungulia milango ya kuondoka Camp Nou.
"Amedumu katika kikosi cha kwanza kwa miaka mingi na anayo haki ya kuamua (kubaki ama kuondoka). Tutaheshimu maamuzi yake," Bartomeu alisema.
"Siku atakayoondoka, ataacha historia kama mchezaji bora kuliko wote waliopitia (Barcelona). Kama anataka kubaki nasi, tutafurahi, kama anataka kuondoka tutamsaiddia.
"Xavi atarejea hapa kwasababu atakuwa kucha mkubwa," aliongeza.
Barca ilimtambulisha kiungo mpya Ivan Rakitic Jumanne waliyemsajili kwa euro milioni 20 kutoka Sevilla.

No comments:

Post a Comment