STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 12, 2013

Rooney kuwakosa Liverpool kesho Uingereza

Mshambuliaji nyota wa Manchester United, Wayne Rooney



LONDON, England
MFUMANIA nyavu mahiri wa Manchester United,  Wayne Rooney kesho ataukosa mchezo Ligi Kuu ya England dhidi ya Liverpool baada ya kushindwa kupona jeraha lake la kifundo cha mguu amesema kocha wa timu hiyo Alex Ferguson.
Rooney aliumia kwenye mazoezi na kukosa michezop yote ya kipindi cha sikukuu dhidi ya Newcastle United, West Bromwich Albion na Wigan Athletic pamoja na mchezo waliotoka sare wa kombe la FA dhidi ya West Ham United.
"Wayne Rooney bado ataendelea kuwa nje ya uwanja ," Ferguson aliwaambia waandishi wa habari. "Natumaini leo ataanza mazoezi mepesi kwa maana hiyo hatachukua muda mrefu kuanzia sasa kurejea uwanjani. Sidhani kama hilo ni tatizo lakini tutakiwa kimlinda.
"Nategemea atakuwa tayari kurejea uwanjani kwenye mchezo wetu wa Jumatano wa marudiano (Dhidi ya West Ham).
Winga Nani na kiungo  Anderson wote wanarejea kikosini kuwakabili Liverpool kwenye uwanja wa Old Trafford.
"Nani ameanza mazoezi na atajumuishwa kwenye kikosi kwa ajili ya mchezo wa Jimapili (kesho).
"Anderson amerejea mazoezini kwa siku kumi sasa hivyo atakuwepo kikosini kwa ajili ya mchezo wa Jumapili. Lakini yote kwa yote tupo katika hali nzuri na ni vizuri kuwa nao kikosini wote.
United wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba nyuma ya majirani zao Manchester City baada ya kucheza michezo 21 na wapo mbele kwa pointi 14 dhidi ya Liverpool wanaoshika nafasi ya nane.
Furgeson alisema kuwa upinzani na Liverpool aubadiliki na siku zote mchezo dhidi yao (Liverpool) ni muhimu kwa kuwa unavuta hisia za mashabiki.

No comments:

Post a Comment