STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 12, 2013

Kitale azidi kumlilia Sharo Milionea

Kitale katika pozi zake matata

Kitale akiwa na Sharo Milionea katika moja ya kazi walizowahi kuzifanya pamoja
MSANII wa fani ya maigizo na muziki, Mussa Yusuf 'Kitale' amesema itamchukua muda mrefu kumsahau swahiba wake, Hussein Mkiety 'Sharo Milionea' kwa namna walivyokuwa wamezoeana na kufanya kazi pamoja.
Alisema namna rafikiye alivyofariki ghafla huku wakiwa wamejipanga kufanya mambo kadhaa ya kimaisha na kisanii ndiyo yanayomfanya kila mara kukumbwa na jinamizi la kumlilia Sharo, aliyefariki kwa ajali ya gari akielekea Tanga.
Alisema yeye na Sharo walikuwa zaidi ya marafiki, ndiyo maana analizwa na kifo cha msanii huyo aliyekuwa akizidi kupaa kwa umaarufu kwa 'swaga' zake za 'Ooh Mamaaaa', 'Kamata Mwizi Meen', 'Umebugi Meen' na nyingine.
"Ni vigumu kumsahau Sharo Milionea, alikuwa zaidi ya rafiki...kibaya zaidi tulikuwa na mambo mengi tumeyapanga kuyafanya ambayo baadhi tulishayaanza na mengine ndiyo hivyo yameishia njiani," alisema Kitale.
Kitale alisema kwa sasa anafanya mipango ya kuachia kazi mbili alizozifanya na Sharo filamu iitwayo 'Impossible' na wimbo uitwao 'Hili Toto'.

No comments:

Post a Comment