STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 12, 2013

Azam bila Kipre Tchetche kuivaa Tusker leo Zanzibar

Kikosi cha mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam Fc
Kikosi cha mabingwa wa Kenya, Tusker

TIMU ya soka ya Azam inatarajiwa kuvaana na Tusker ya Kenya katika pambano la fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi bila ya mshambuliaji wake nyota, Kipre Tcheche, ingawa inafurahia kurejea kwa kiungo wao, Abdulhalim Humud 'Gaucho'.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo, itaumana na Tusker katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar, huku uongozi wa klabu hiyo ukitamba umejipanga kutetea taji hilo licha ya kukiri itakuwa mechi itakuwa ngumu.
Mabingwa hao watetezi walipata nafasi hiyo kwa kuing'oa Simba katika mechi ya fainali kwa mikwaju ya penati 5-4 baada ya kutoka sare ya 2-2 katika muda wa dakika 120 wakati Tusker walifuzu juzi kwa kuilaza Miembeni kwa mabao 2-0.
Azam itashuka dimbani bila ya nyota wake Kipre Tchetche aliyeumia katika pambano dhidi yao ya Coastal Union, japo karibu kikosi chake chote kipo imara hasa baada ya kurejea kwa kiungo nyota, Abdulhalim Humud 'Gaucho'.
Afisa Habari wa Azam, Jafar Idd 'Mbunifu' alisema kurejea kwa Humud kumewapa faraja na matumaini makubwa ya kutetea ubingwa huo walioutwaa mwaka jana kwa kuilaza Jamhuri ya Pemba mabao 3-0.
Idd alisema licha ya kutarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Tusker aliokiri ni moja ya timu ngumu isiyotabirika, lakini wamejipanga kutetea ubingwa wao kwa mara ya pili mfululizo.
"Kwa kweli tumejipanga vema, japo hatutakuwa na Kipre Tchetche aliye majeruhi, lakini kocha John Stewart Hall amemuita Humud aliyepona ambaye ameshatua mjini hapa tayari kwa pambano hilo la kesho (leo) dhidi ya Tusker," alisema Idd.
Kwa mujibu wa rekodi za michuano hiyo ni Yanga pekee iliyowahi kutetea taji kwa kulitwaa mara mbili mfululizo, ilivyofanya hivyo mwaka 2004 na 2005, wakati miaka mingine yote kila anayetwaa taji hilo hushindwa kulitetea.
Mabingwa waliopita wa michuano hiyo ni;
2003-Mtibwa Sugar
2004-Yanga SC
2005-Yanga SC
2006-Simba SC
2007-Yanga SC
2008-Simba SC
2009-Miembeni FC
2010-Mtibwa Sugar
2011-Simba FC
2012-Azam FC
2013   ???

No comments:

Post a Comment