STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 12, 2013

OMBAOMBA FEKI ATIMKA BAADA YA KUGUNDULIKA SIO MLEMAVU


Baada ya kugundua wananchi wamemshtukia baada ya kumhoji maswali na kushindwa kujibu aliamua kutimua mbio kukwepa kamera ya Francis Godwin isimpate picha yake, kama unavyomuona hapo mdau mguu gafla umetokea kimiujiza pamoja na mkono, yote hiyo alikuwa ameificha kwa kutumia koti lake na Suruali alizovaa. 
Baada ya hali kuwa tete alijikuta anazisaha umpaka kandambili zake, kama unavyoziona. 
Huyu ni omba omba anayeigiza kutokuwa na mkono mmoja na mguu Mmoja akiwa amekaa eneo la M.R Iringa mjini akisubiri kuomba chochote kutoka kwa wapita njia leo.

ULE usemi wa wahenga kuwa ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni, ulitimia katika eneo la M.R,  mjini Iringa baada ya wananchi waliokuwepo eneo hilo kupigwa na butwaa baada ya ombaomba marufu anayefahamika kama Mzee Janja anayeshinda katika eneo hilo akijifanya mlemavu aliyekuwa na mkono na mguu mmoja mmoja, kutimua mbio kukwepa kamera ya mapaparazi mjini humo.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 8 mchana baada ya kamera ya mtandao wa Francis Godwin kufika eneo hilo la kushuhudia umati wa wananchi wakiendelea kumpa fedha Mzee Janja, ambaye walikuwa wakidhani ni mlemavu wa viungo, na anayeongea kwa tabu..
Hata hivyo baada ya mmoja kati ya wananchi kufika eneo hilo alionyesha kufichua mbinu hiyo chafu ya mzee huyo kujifanya ni mlemavu wakati asubuhi alikutana nae maeneo ya mjini akiwa mzima wa afya njema na katika kumhoji zaidi ndipo kamera ya mtandao huo ilipoamua kufanya kazi yake ya kunasa kituko hicho na ndipo mzee huyo alipoanza kuongea kwa sauti vizuri tofauti na alivyokuwa akijifanya kuwa hawezi kuongea kabisa (bubu)

Wakati mabishano yakiendelea eneo hilo ghafla mzee huyo alisimama kwa miguu yake yote miwili pamoja tofauti na  awali alivyokuwa akijifanya ni mlemavu asiye na mguu mmoja ila baada ya watu kutaka apigwe picha ndipo mzee huyo alipoanza kutimua mbio huku ulemavu aliokuwa nao akiusahau hapo pamoja na kandambili zake na hakuna mtu aliyeweza kumfukuza na kufanikiwa kumkuta.

Baadhi ya wananchi wameuomba uongozi wa Manispaa ya Iringa kuwabana omba omba hao ambao wamekuwa wakidanganya watu kuwa wao ni walemavu kumbe ni wazima na kutaka kuwepo kw

No comments:

Post a Comment