STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

Uholanzi yaingia Tano Bora, Tanzania yapaa FIFA

WAKATI Tanzania ikizidi kupaa katika viwango vya ubora wa soka duniani kutoka nafasi ya 116 hadi 109 ikiwa na maana imepanda nafasi saba, nchi ya Uholanzi imefanikiwa kuingia kwenye Tano ya orodha mpya iliyotangazwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka, FIFA, huku nchi ya England ikiporomoka kwa nafasi mbili.
Katika orodha mpya nafasi nne za juu imeendelea kubaki vile vile kama ilivyokuwa mwezi uliopita ambapo Hispania ianongoza , ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Croatia.
Ureno ya Cristiano Ronaldo imeshuka kwa nafasi mopja hadi nafasi ya sita, ikifuatiwa na Colombia, Italia, England na Ecuador.
Kwa ukanda wa Afrika Ivory Coast wameendelea kuongoza orodha ikiwa nafasi ya 13 duniani ikifuatiwa na Ghana iliyopo nafasi ya 21 duniani na Mali (23).
Ukanda wa Afrika Mashariki na kati, Uganda inaongoza ikishika nafasi ya 24 Afrika na 93 duniani ikifuatiwa na Ethiopia, kisha Tanzania iliyopanda kwa nafasi saba hadi nafasi ya 109 duniani na 32 Afrika.
Inayofuata baada ya Tanzania ni Kenya iliyolala jana 1-0 kwa Nigeria, kisha Burundi, Rwanda, Sudan, Eritrea, Sudan Kusini, Somalia na Djhibout inayoshika mkia.

No comments:

Post a Comment