STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 6, 2013

Hatimaye Ngwair apumzishwa nyumba yake ya milele

BAADA ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, hatimaye mwili wa msanii Albert Mangweha 'Ngwair' umepumzishwa leo katika nyumba yake ya milele katika makaburi ya eneo la Kihonda Morogoro.


Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri, ambapo
Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita. 
Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.
16f11344cea711e2813a22000a1f8f34_7
75e8603ecea511e29ecd22000aaa08de_7
4406673ccea511e2850422000a1f9a85_7
“Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa sana ni umati usioelezeka mungu akulaze mahali pema peponi,” ameandika Izzo B kwenye Instagram.

Naye Lady Jaydee kupitia Twitter ameandika: Mpk hapa tulipomsindikiza panatosha. Mungu amrehemu, kazi tumeimaliza. Life goes on.”
e1147594cea211e2a86422000a1f9839_7
ee9d94facea411e2a9ea22000ae81462_7
f18745b2cea411e2aa3022000a9e2931_7



Aidha msanii aliyekuwa na Ngwair nchini Afrika kusini Mgaza Pembe maarufu kama M to the P, naye alifanikiwa kutimba nchini na kumuaga 'swahiba' wake kabla ya kuzikwa baada ya awali kufichwa ukweli kuhusu kiofo cha mwenzake.

M to the P aliyekuwa amelazwa hoi hospitalini wakati Ngwair akiaga dunia, aliwasili nchini baadaya kupata ukweli wa mwenzake baadaya awali kufichwa kuwa ametangulia Dar wakati yeye alipokuwa hoi hospitalini na alishindwa kujizuia kumlilia rafikiye huyo wakati akiuaga mwili wa Ngwair leo mchana.
Inaelezwa alipewa taarifa na rafikie wa kike aitwaye Maggie baada ya kumdodosa sana ukweli kuhusu Ngwair na namna waliokuwa wakimtembelea hospitali alikolazwa walivyotoweka ghafla.
Chanzo:Mpekuzi Huru

No comments:

Post a Comment