STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 24, 2013

TP Mazembe yamnyakua kocha wa Mali


https://lh6.googleusercontent.com/-VEtRhDY7qrI/UZzx8PeR2fI/AAAAAAAAlAE/izjc83pUpI8/patrice-carteron-dijon5.jpg?imgmax=800
Kocha Patrice Carteron

LUBUMBASHI, Congo DR
KAMPENI za Mali za kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zilipaa juzi Jumatano wakati kocha wao Patrice Carteron  aliposaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya TP Mazembe ya Congo.
Mali, ambayo chini ya kocha huyo Mfaransa ilimaliza ya tatu katika fainali ya Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini, ina mechi za kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Rwanda na Benin Juni 9 na Juni 16.
"Tunamtambua Patrice Carteron kama kocha wa Mali," rais wa shirikisho la soka la nchi hiyo Hamadoun Kola Cisse alisema katika mahojiano na kituo cha radio cha Ufaransa.
"Yuko katika mkataba hadi mwakani lakini kwa kwenda kusaini mkataba mwingine anajiweka matatani," Cisse alisema.
Katika muda huo huo wa mahojiano, beki wa zamani wa klabu za St Etienne na Sunderland, Carteron (42) alikuwa alikuwa akitambulishwa hadharani kwenye Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi.
"Hatuna pingamizi kwa Carteron kuiongoza Mali katika mechi zao mbili zijazo Juni licha ya kusaini mkataba nasi," mwenyekiti Moise Katumbi alisema.

No comments:

Post a Comment