STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 19, 2013

Mabao 58 yafungwa Ligi Kuu, Tambwe nouma Ashanti, Prisons angalau sasa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSAUn1hwkMI3BcBcVeWb4YPc0cKNG2217o1rBuA9t_YRDuDqEfojRYqpc29if8_8ljHN5fIIGwDFx3hdNQ8y8cAo4E9tHnw8BP3Wr4L1T4iGcr2gWQ3Ua9aWJGULdoHdk_r9la7cxPVzw/s1600/DSC_0072.jpg
Tambwe Amissi

JUMLA ya mabao 58 yametinga wavuni mpaka sasa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa imemaliza raundi nne tangu ilipoanza rasmi Agosti 28 mwka huu, huku Mrundi Tambwe Amisi akiongoza orodha ya wafungaji baada ya jana kutupia mabao manne pekee yake wakati Simba ikiichinja Mgambo JKT kwa mabao 6-0.
Mfungaji Bora huyo wa michuano ya Kombe la Kagame, anafukuziwa na wachezaji wa Yanga na Simba, Jerry Tegete na Haruna Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja, huku wachezaji sita wengine wakiwa kwenye nafasi ya tatu na mabao mawili kila mmoja.
Wachezaji hao ni Didier Kavumbagu wa Yanga, Saad Kipanga wa Rhino Rangers, Bakar Kondo wa JKT Ruvu, Elias Maguri (Ruvu Shooting), Jonas Mkude wa Simba na Jerry Santo (Coastal Union).
Safu ya mbele ya Simba ndiyo mpaka sasa inaonekana kuwa kali baada ya kutumbukiza wavuni mabao 11 ikifuatiwa na watani zao Yanga wenye mabao nane, huku timu ya Prisons ndiyo yenye safu butu ya ushambuliaji ikitupia bao moja tu wavuni, ikizidiwa na timu za Oljoro JKT na Ashanti yenye mabao mawili kila moja.
Wakati ukuta wa JKT Ruvu ukiwa mgumu kupitika, ule wa maafande wenzao wa Mgambo JKT ndiyo 'nyanya' baada ya kuruhusu mabao 9 mpaka sasa ikifuatiwa na Ashanti (8) na Prisons iliyofungwa mabao 7.
Mashabiki wa soka watarajie mabadiliko makubwa ya orodha ya ufungaji na hata kwenye msimamo wa Ligi Kuu ambao kwa sasa unaoongozwa na Simba mwishoni mwa wiki wakati ligi hiyo itakapoendelea kwa timu zote 14 kushuka tena dimbani, huku pambano linalosubiriwa kwa hamu likiwa ni Yanga na Azam.
Chini ni msimamo wa sasa wa Ligi hiyo na orodha ya wafungaji mabao;

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                            P  W  D  L    F  A  GD  PTS
1. Simba                         4   3   1   0   11 2  9   10
2. JKT Ruvu                   4   3   0   1   6  1   5    9
3.  Ruvu Shooting           4   3   0   1   6  2   4    9
4.  Yanga                        4   1   3   0   8  4   4    6
5.  Azam                         4   1   3   0   5  3   2    6
6.  Coastal Union            4   1   3   0   4  2   2    6
7.  Mbeya City                4   1   3   0   3   2   1   6
8.  Kagera Sugar             4   1   2   1   3   3   0   5
9.  Mtibwa Sugar            4   1   2   1   2  3   -1   5
10.Rhino Rangers            4   0   3   1   4  6   -2   3
11. Mgambo JKT           4   1   0   3   1   9  -8   3
12. Prisons                      4   0   2   2   1   7  -6   2
13. Oljoro  JKT              4   0   1   3   2   6  -4   1
14. Ashanti United           4   0   1   3   2   8  -6   1

Wafungaji:

4- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete (Yanga), Haruna Chanongo (Simba)
2- Didier Kavumbangu (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Jerry Santo (Coastal Union)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, (Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel, Salim Majid (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, Kipre Tchetche (Azam), Mwagane Yeya, Steven Mazanda, Paul Nonga (Mbeya City), Laurian Mpalilem, Peter Michael (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga (Mgambo JKT), Themi Felix, Godfrey Wambura, Maregesi Marwa (Kagera Sugar), Amir Omary, Shaibu Nayopa (Oljoro JKT)

Matokeo ya mechi za awali


Agosti 24, 2013
Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013

Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)


Sept 18, 2013
Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Ratiba ya mechi zijazo mwishoni mwa wiki hii
Jumamosi
Mgambo JKT vs Rhino Rangers
Prisons vs Mtibwa Sugar
Simba vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Ashanti United

Jumapili:

 JKT Ruvu vs Oljoro JKT
Azam  vs Yanga
Coastal Union v Ruvu Shooting 

No comments:

Post a Comment