STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 18, 2013

Ray, Lulu kunogesha Dar Filamu Festival 2013

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AO9WimIAAAfiUjk68wAAAJhFJXY&midoffset=2_0_0_1_1304473&partid=5&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331
Stanford Kihore (kati) akizungumza huku Lulu kushoto akiwa makini
TASNIA ya filamu Tanzania inakua kwa kasi sana kila kunapokucha lakini pengine ni tasnia pekee ambayo imekuwa na changamoto nyingi, na sintofahamu kwani ndio tasnia ambayo imekosa mtiririko wa matukio ambayo huwa kama motisha kwa wadau na wasanii wa filamu kwa muda mrefu tasnia ya filamu hakuna tuzo zozote takribani miaka sita zilipofanyika tuzo za Vinara 2007/8.

Tuzo na matamasha ya filamu ni vitu ambavyo uchochea sana ubora na ukuaji wa filamu katika tasnia ndio maana sehemu yoyote yenye mafanikio ya filamu lazima utawaliwa na matamasha ya sinema, ukiangalia filamu za kibongo ni nyingi sana na zimekuwa zikizalishwa na kutolewa kwa wingi na kuingia sokoni kwa kasi bila kuwa na mizania yoyote jambo linalotuchelewesha na kushindwa kufikia medani za kimataifa.

Hivi karibuni tamasha kubwa la filamu limezinduliwa na linatarajia kufanyika kuanza tarehe 24 hadi 26 Septemba 2013 katika viwanja wa CoICT- UDSM- Posta Kijitonyama Tamasha litaambatana utoaji wa  Semina kwa wadau wa filamu, kuonesha filamu za kitanzania kwa watu wote bure kwa siku tatu,Kutakua na filamu nne kwa siku kuanzia saa kumi na mbili jioni mpaka saa tano usiku.

Tamasha hilo linaloitwa Dar Filamu Festival (DFF 2013/14) linajenga histori mpya katika tasnia ya filamu kutokana na sera ya tamasaha lenyewe ambalo limekusudia kutoa fursa na kuwajengea uzoefu watayarishaji wa filamu sambamba na wasanii na kubaini umuhimu wa kuwa na matamasha, DFF pia imekusudia kutumia fursa ya kufanya Lugha ya Kiswahili bidhaa yenye mlengo wa kibiashara.

Filamu zitakazoonyeshwa ni zile ambazo zimetumia kuigizwa kwa Lugha ya Kiswahili tu, kwa kuanza ni filamu za Tanzania tu ndiyo zitakazorushwa katika Projecta kubwa kwa siku tatu  kwa jioni kuanzia saa kumi na mbili hadi saa tano usiku, hiyo ni sehemu muhimu sana na kubwa kwani hiyo ni fursa nyingine ya kuongeza mauzo badala ya njia moja tu ya kuuza Dvd pekee.

Ni Tanzania pekee ndiyo ambayo utegemea sana mauzo ya aina moja tofauti na nchi zilizoendelea ambazo kuna aina nyingi za ufanyaji wa biashara ya filamu, ikiwa soko kama uuzaji wa filamu katika majumba ya sinema tukio ambalo huwa la kwanza kabisa, filamu kuonyeshwa awali kabisa kabla ya kuingia  mtaani, filamu ikitoka kila kitu ni biashara.

Katika Dar Filamu Festival 2013/14 inastahili pongezi kwani pia inajenga hadhi kwa waigizaji wetu tayari wasanii ambao wamekuwa na mchango mkubwa wanakuwa mabalozi wa tamasha hilo, msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ anasimama kama mwigizaji wa kike anayewakilisha wasanii wenzake kama balozi anayebeba wengine na alama ya tamasha .

Balozi mwingine Vincent Kigosi ‘Ray’ ambaye akiwa kama mtayarishaji na muongozaji aliyechangia ukuaji wa tasnia ya filamu Tanzania, tamasha limempa nafasi kama official Producer and Director  kwa tamasha kuwaweka mbele wasanii wetu ni njia nyingine ya biashara kwao, mara nyingi kuna changamoto nyingi kwa wasanii wetu pamoja na kuwa na wafuasi wengi bado hawapati nafasi za matangazo.

“Nimefurahia sana kuchaguliwa kama Balozi wa Dar Filamu Festival na ninafuraha sana kwani kwanza kabisa ni kuonyesha uzalendo kwa kuwa na tamasha la filamu linalotuhusu sisi kama watengenezaji filamu za Kiswahili Lugha ambayo wenzetu wakenya na nchi nyingine wanakitumia vizuri na kuwaingizia fedha, huku sisi tukibaki maskini,”anasema Ray.

Mratibu wa tamasha hilo Staford Kihore anasema kuwa katika kufanikisha hilo DFF inakuwa ni chachu ya maendeleo ya tasnia ya filamu Tanzania, huku tukisema kuwa Dar Filamu Festival 2013 kwa kauli mbiu ya ‘Ubora wa Filamu Zetu’ ikiwa ni njia ya kuwakutanisha wadau wote kwa pamoja na kuwa jukwaa linalojenga tasnia ya filamu inayokua kila siku huku pia tamasha likitoa njia nyingine ya soko jipya.

“Kwa tamasha hili la awali tutaonyesha filamu za hapa Tanzania pekee ikiwa ni utambulisho wa Dar Filamu Festival kwa mara ya kwanza kwenu wanahabari, miaka ijayo Tamasha litahakikisha linashirikisha filamu kutoka sehemu mbalimbali zinazotumia Lugha ya Kiswahili  kutoka popote Ulimwenguni,” anasema Staford Kihore.

“Mimi kama Balozi wa Dar Filamu Festival ninaona fahari sana kwa ukuaji wa tasnia ya filamu tunaomba watu waliunge mkono tamasha hili kwani sisi tunapiga hatua katika tasnia ya filamu, wadau waje katika viwanja vya Posta wajionea filamu pia filamu yangu ya Foolish Age itaonyeshwa tena bure kabisa nashukru sana kuchaguliwa waigizaji tupo wengi,”anasema Lulu.

Akiongea na FC mratibu wa Tamasha hilo Staford Kihore pia amesema kuwa katika kuzingatia maendeleo ya tasnia ya filamu siku tatu hizo kila siku imepewa jina kwa filamu zitakazoonyeshwa kuanzia Tarehe 24th September, 2013 siku ya Jumanne ambayo ndio siku ya ufunguzi utakuwa ni usiku wa Bongo Movie Classics, 25th September, 2013 ni usiku wa Quality Nights.

Na ile siku ya mwisho tarehe 26th September, 2013 itakuwa ni Stars Nights siku ambayo kutakuwa na wasanii wetu mbalimbali ambao wanajenga soko hilo la Bongo movie filamu, Tamasha hili linapambwa na wasanii wote wakiwakilishwa na wasanii wenzao wawili ambao ni Vincent Kigosi ‘Ray’ kama Official Producer and Director  for DFF 2013 na Elizabeth Michael ‘Lulu’ kama Official Actress for DFF 2013.

Pia tamasha litaambatana na utoaji wa semina kwa wadau wa filamu kwa asubuhi ambapo madarasa  yataendeshwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sanaa tarehe 24 September, 2013 masomo ya Uandishi wa Muswada, Uigizaji na  Uongozaji wa filamu yatafundishwa kwa washiriki, 25th September 2013 Siku nzima Makapuni ya Utengenezaji filamu yataonyesha na kutangaza kazi zao kwa wadau mbaliambali.

Tarehe 26th September 2013 ni siku muhimu sana kwani Taasisi kama vile TRA, Bodi ya Ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza, Wasambazaji wa filamu na taasisi nyingine watakutana katika jukwaa la majadiliano kuhusu mustakabali wa tasnia ya filamu, pia filamu kadhaa zitaonyeshwa na kujadiliwa na wadau watakaokuwepo matukio yote ya asubuhi yatafanyika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Sanaa.

Kampuni ya Haak Neel Production na Filamucentral mtandao wa habari za filamu ndio waandaaji  wa tamasha hilli la Dar Filamu Festival (DFF) 2013,  kwa kushirikia na taasisi kama Bodi ya Filamu na ukaguzi wa michezo ya kuigiza Tanzania, Tanzania Film Federation (TAFF), UDSM- PFA, MFDI, Swahiliwood, Global Publishers.

Na makapuni ya usambazaji wa filamu Steps Entertainment Ltd, Leo Media na kampuni mpya ya usambazaji ya Proin Promotion ambayo imeanza hivi karibuni na kuonyesha dhamira ya kusaidia tasnia ya filamu, pia unaweza kupata habari zaidi kupitia mtandao wa www.dff.or.tz

Baada ya kuja tamasha la filamu ambalo limepokelewa vema na wadau wote ni kama moja ya kuelekea katika Nyanja za kimataifa ni wakati ambao pia Serikali na taasisi nyingine kuunga mkono na kuhamasisha uwepo wa tuzo za ndani, ambazo hazipo kwa muda mrefu tofauti na fani ya muziki ambayo kila aina yake imekuwa na tuzo, pia hivi karibu wadau walikutana kwa kujadili suala la sera ya Filamu.

Kwa shirikisho la wasanii wa filamu Tanzania (TAFF) kuweka mjadala huo ni hatua mojawapo wa kufungua njia ya kuelekea katika medani za kimataifa, pengine sera ya filamu ikiwepo itasaidia tasnia ya filamu kukua zaidi na kuwa rasmi tofauti na ilivyo sasa wadu wadai hivyo.

No comments:

Post a Comment