STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 18, 2013

Tambwe aanza mambo Simba, JKT chali, Azam, Yanga mmmh!

Mrundi Tambwe Amisi akishangilia moja ya mabao yake leo uwanja wa Taifa (Pix:Bin Zubeiry)
MABAO manne ya nyota wa kimataifa wa Simba, Tambwe Amisi kutoka Burundi yameiwezesha Wekundu wa Msimbazi kukalia usukani wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuitafuna Mgambo JKT kwa mabao 6-0.
Simba ilipata ushindi huo mnono kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kufikisha jumla ya pointi 10 na mabao 11 ikiwaengua JKT Ruvu iliyokuwa ikiongoza.
Simba imekwea kileleni baada ya waliokuwa vinara JKT Ruvu kulala bao 1-0 mbele ya ndugu zao Ruvu Shooting katika pambano jingine lililochezwa kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi.
Mabao mengine ya leo ya Simba yaliwekwa kimiani mshambuliaji anayezidi kuja juu nchini wa klabu hiyo ya Simba, Haruna Chanongo. Kwa kufunga mabao hao manne Tamwe ameweka rekodi ya aina yake ya kuwa mchezaji wa kwanza kwa misimu mitatu kufunga zaidi ya mabao mawili katika mechi moja pia kukwea kwenye nafasi ya kwanza ya ufungaji mabao akiwaacha nyuma akina jerry Tegete na Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja.
Wakati Simba ikichekelea ushindi huo wa kishindo jijini Dar mabingwa watetezi Yanga waliokuwa mjini Mbeya walijikuta wakipata sare ya tatu mfululizo baada ya Prisons kuwagomea.
Jerry Tegete alitangulia kuipatia bao Yanga kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 77 kupitia Peter Michael na kufanya mechi hiyo iliyochezw auwanja wa Sokoine kuisha kwa sare ya 1-1.
Waliokuwa vinara wa ligi hiyo, JKT Ruvu walijikuta wakiangukia pua mbele ya Ruvu Shooting kwa kulazwa bao 1-0 katika mechi iliytochezwa uwanja wa Mabatini, Pwani.
Katika pambano jingine lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, wenyeji Azam ilijikuta wakilazimishwa sare ya bao 1-1 na Ashanti United.
Azam walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia mfungaji bora wa ligi iliyopita, Kipre Tchetche dakika ya 20 ya mchezao kabla ya Anthony Matangalu kuisawazishia Ashanti dakika ya 78.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo Coastal Union ikiwa jijini Tanga imenusurika kipigo baada ya nahodha wake Jerry Santo kusawazisha bao na kufanya wagosi hao wa Kaya kutoka sare ya 1-1 na Rhino Rangers ya Tabora.
Nao Kagera Sugar wakiwa nyumbani kwao uwanja wa Kaitaba walmechomoza na ushindi wa mabao 2-1 dakika za jioni dhidi ya JKT Oljoro, huku Mtibwa Sugar kwenye uwanja wao wa Manungu, walibanwa mbavu na Mbeya City na kwenda nao suluhu ya kutofungana.

No comments:

Post a Comment