STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 6, 2018

Yanga yarahisishiwa kazi Kombe la Shirikisho Afrika

Yanga SC ambao muda mchache ujao watalianzisha kwa USM Alger katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika.
KIGALI, RWANDA
WAKATI Yanga ikijiandaa usiku huu kuvaana na USM Alger mjini Algiers, Algeria, wapinzani wao katika kundi hilo, Rayon Sports ya Rwanda na Gor Mahia ya Kenya wameshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 mjini Kigali, Rwanda.
Katika pambano hilo klililochezwa Uwanja wa Nyamirambo, wageni Gor Mahia ndio waliokuwa wa kwanza kuandika bao dakika ya 10 likifungwa na Mnyarwanda Meddie Kagere kabla ya wenyeji kuchomoa kupitia Eric Rutanga dakika ya 24.
Matokeo hayo yametioa nafuu kwa Yanga katika mbio zao za kuwania kutinga robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kundi lao, lakini ikitegemeana na matokeo yake ya usiku huu nchini Algeria.
Baada ya mchezo wao wa usiku huu, Yanga itarudi nyumbani kuisubiri Rayon katika mechi yao ya pili, wakati Gor Mahia itakuwa mjini Nairobi kuipokea USM Alger mechi zikichezwa Mei 16.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, ASEC Mimosas iliwatambia Aduana Stars ya Ghana kwa bao 1-0 mjini Abidjan, Ivory Coast, Berkane ya Morocco nayo ilishinda 1-0 dhidi ya Al Hilal Omdurman ya Sudan na Enyimba ikiwa nyumba Nigeria iliwatmbia Djoliba ya Mali kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment