STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 5, 2018

Ajibu atupia kambani, Yanga 1-0 Taifa Jang'ombe

RAHIM JUNIOR
IBRAHIM Ajib ameitanguliza Yanga mguu mmoja kwenye nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika chache kabla ya kwenda mapumziko akimalizia mpira wa shuti kali ha Yohana Nkomola kuokolewa na kipa wa Jang'ombe.
Kwa sasa pambano hilo lipo mapumziko na kama matokeo yatasalia hivyo, basi Yanga itaifuata Singida United iliyotangulia mapema leo mchana kwa kuilaza Mlandege.
Katika mchezo wa leo unaochezwa Uwanja wa Amaan usiku huu, Yanga imechezesha kikosi cha vijana zaidi, huku wakongwe kama kina Youthe Rostand, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amissi Tambwe, Papy Kabamba Tshishimbi wakiwa jukwaani.

No comments:

Post a Comment