STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 5, 2018

Singida United yatangulia nusu fainali, Azam yatibuliwa Mapinduzi Cup

Kikosi cha Azam ambacho jioni hii kimelala mbele ya URA

Wachezaji wa Singida wakipongezana katika mechi yao ya Kombe la Mapinduzi

Danny Usengimana akijiandaa kupioga penalti iliyoiandikia Singida bao la kuonmgoza jioni ya leo
TARIQ JUNIORVIJANA wa Hans Pluijm, Singida United sio wa mchezo mchezo, baada ya jioni ya leo kuwa timu ya kwanza kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2018 kwa kuichakaza Mlandege kwa mabao 3-0, huku Azam ikitenguliwa udhu na Watoza Ushuru wa Uganda.
Singida imefikisha pointi 9 ikiwa imecheza mechi tatu na kukata tiketi moja ya Kundi A ambalo lina timu ya Yanga inayoshuka dimbani usiku huu kuumana na Taifa Jang'ombe katika mechi nyingine kali ya michuano hiyo.
Walima Alizeti hao wamejihakikishia nafasi hiyo kutokana na ukweli timu zilizopo nyuma yake ni Yanga pekee inayoweza kuzipiku pointi ilizonazo, huku pia ikiwa na michezo miwili mkononi ya kufungia makundi.
Mabao ya Danny Usengimana aliyefungwa kwa penalti dakika ya 29 na mengine Kenny Ally la dakia ya 37 na lile la Lubinda Mundia la dakika ya 56 yalitosha kuipa ushindi Singida inayoshiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza mwaka huu.
Wakati Singida ikichekelea kutangulia nusu fainali, watetezi wa taji hilo, Azam ilinyooshwa na URA ya Uganda kwa bao 1-0 na kutenguliwa rekodi yao iliyokuwa ikishikilia kwa kutoruhusu bao lolote tangu michuano ya 2017.
Azam ilibeba taji hilo Januari mwaka jana kwa kucheza mechi zake zote bila kuruhusu bao lolote achilia mbali kupoteza mchezo, lakini URA wakiwa na utulivu mkubwa waliwaotea Matajiri nao na kuwatengua 'udhu' kwa bao la dakika ya 32 lililofungwa na Nicholaus Kabaga akipiga tobo kipa Razak Abalora.
Hata hivyo Azam bado ina nafasi ya kupenya hatua ya nusu fainali kama itapata matokeo mazuri katika mechi yao ya mwisho kesho dhidi ya Simba ambayo inafuatia nyuma yao kwa alama zao nne baada ya kucheza mechi mbili.
URA imefikisha pointi saba na kuongoza msimamo wa kundi hilo la B, kisha Azam ikifuata na alama zao 6. Timu zote tatu zina nafasi sawa ya kutinga nusu fainali kupitia kundi hilo na zinatarajiwa kukutana zenyewe kuamua hatma yao.
Cheki matokeo ma msimamo mzima wa michuano hiyo inayoingia mwaka wa 11 tangu kuasisiwa kwake mnamo Mwaka 2007;
Kombe la Mapinduzi 2018
Kundi A
Mlandege, JKU, Zimamoto, Yanga, Taifa Jang'ombe, Singida United

Kundi B
Jamhuri, Mwenge, Simba, Azam, URA

Des 29, 2017
Mlandege 2-1 JKU
Jamhuri 0-1 Mwenge
Zimamoto 2-1 Taifa Jang’ombe

Des 30, 2017
Zimamoto 0-1 JKU
Taifa Jang’ombe 1-0 Mlandege

Des 31, 2017
Azam 2-0 Mwenge
Jamhuri 1-1 URA

Jan 01, 2018
Mlandege 2-1 Zimamoto
JKU 0-0 Taifa Jang’ombe

Jan 02, 2018
Singida United 3-2 Zimamoto
Simba 1-1 Mwenge
Yanga 2-1 Mlandege

Jan 03, 2018
URA 1-0 Mwenge
Azam 4-0 Jamhuri
Taifa Jang’ombe 1-3 Singida United

Jan 04, 2018
JKU 0-1 Yanga
Simba 3-1 Jamhuri

Jan 05, 2018
Mlandege 0-3 Singida United
URA 1-0 Azam
Yanga v Taifa Jang’ombe

Jan 06, 2018JKU v Singida United
Simba v Azam

Jan 07, 2018Zimamoto v Yanga

Jan 08, 2018Simba v URA
Yanga v Singida United

Nusu FainaliJan 10, 2018Kinara Kundi A v
Mshindi wa Pili Kundi B

Kinara Kundi B v
Mshindi wa Pili Kundi A
Saa 2:15 usiku

FAINALIJan 13, 2018Saa 2:15 usiku

Msimamo:
Kundi A
               P   W   D    L   F   A    Pts
 

1.Singida 3    3    0    0    9    3    9
2.Yanga   2    2    0    0    3    1    6
3.M'ndege5   2    0    3    5    7    6
4.Taifa     4    1    1    2    3    5    4
5.JKU      4    1    1    2    2    3    4
6. Z'moto 3    1    0    2    3    4    3

Kundi B
              P   W    D   L    F   A    Pts
 

1.URA     3    2    1    0    3    1     7
2.Azam   3    2    0    1    6    1    6
3.Simba  2    1    1    0    4    1    4
4.Mwenge4    1    1    2    2    4    4
5.Jamhuri4    0    1    3    2    9    1


No comments:

Post a Comment