STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 5, 2018

Yanga, Azam, Singida wasipojipanga wamekwisha Kombe la FA


Kikosi cha Yanga

Azam FC
RAHMA WHITE
VIGOGO wa Ligi Kuu Bara, Yanga, Azam na Singida United, lazima zijipange baada ya kupewa wababe katika mechi za Raundi ya Tatu ya michuano ya Kombe la FA.
Katika droo ya michuano hiyo iliyofanyika asubuhi ya leo ikihusisha timu 32 zilizopenya hatua hiyo, Yanga imepewa wababe wa Mbeya City, Ihefu FC ya Mbalali, huku Singida wakikabidhiwa watemi wea Simba, Green Warriors.
Azam yenyewe imepangwa kupepetana na Shujaa FC katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Mkamba CCM, mjini Morogoro ili kusaka tiketi ya kuingia Robo fainali.
Katika raundi hiyo ya imehusisha timu nne za Mabingwa wa Mikoa (RCL), tatu za Ligi Daraja la Pili (SDL), 12 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na klabu 13 za Ligi Kuu zilizopenya kwenye mechi zao za raundi ya pili zilizochezwa mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mechi za raundi hiyo zitachezwa kati ya Januari 31 na Febaruari Mosi kwenye miji tofauti kulingana na ratiba ilivyo.
Kabla ya mechi hizo za raundi ya tatu kuchezwa tayari zimechezwa mechi 59 na magoli 137 yamefungwa.

Cheki ratiba kamili ilivyo na viwanja vyake:

Kagera Sugar     v Buseresere FC- Kaitaba, Bukoba
Shupavu FC       v Azam FC- Mkamba CCM, Morogoro
Majimaji Rangersv Mtibwa Sugar - Ilulu, Lindi
Kariakoo Lindi     v Mbao FC- Ilulu, Lindi
Prisons               v Burkina Fc- Sokoine, Mbeya
Green Warriors    v Singida FC-Azam Complec, Dar
Mwadui FC          v Dodoma FC- Mwadui, Shinyanga
Ihefu FC              v Yanga SC-Sokoine, Mbeya
JKT Tanzania        v Polisi Dar- Uhuru, Dar
Polisi Tanzania      v Friends- Ushirika, Moshi
Pamba SC            v Stand United-Kirumba, Mwanza
Ndanda FC           v Biashara United-Nangwanda Kiluvya United      v JKT Oljoro-Mabatini, Pwani
Njombe Mji          v Rhino Rangers-Sabasaba Njombe
Majimaji Fc          v Ruvu Shooting -Majimaji, Songea
KMC                    v Toto Africans- Uhuru, Dar

No comments:

Post a Comment