STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 1, 2014

Mwanafunzi wa RUCO aliyechomwa moto Iringa afariki

Mwanafunzi (LEMA) aliyejeruhiwa kwa moto
Mwanafunzi huyu Daniel Lema alikuwa akisoma mwaka wa nne, kozi ya sheria katika chuo kikuu kishiriki cha Mt. Augustino cha Ruaha Iringa (Ruaha University College maarufu kama RUCO).
Mwanafunzi huyo alichomwa moto wiki iliyopita akihusishwa na tuhuma za wizi.
Baada ya kulazwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa kwa wiki moja sasa, mwanafunzi huyo ameaga dunia majira ya saa nane mchana.
Taratibu za kuaga mwili wake zinaendelea kufanywa na uongozi wa chuo hicho, ndugu na wanafunzi wenzake.

Taarifa za awali zinaonesha kwamba mwili wake utaagwa kesho kuanzia saa moja asubuhi kabla ya kusafirishwa kupelekwa kwao mkoani Kilimanjaro kwa mazishi. Mazishi ya kijana huyo yanatarajia kufanyika jumatano ya wiki hii.

Juni 24, mwaka huu Daniel Lema alikutwa na mkasa wa kukamatwa na kuchomwa moto wakati akitoka kuangalia fainali za kombe la dunia katika moja ya Bar za mjini Iringa.

Akiwa amelewa aliingia katika moja ya migahawa ya mjini hapa akitafuta chakula, ilikuwa majira ya saa tano mwanafunzi huyo aliingia kwenye mgahawa ambao biashara hiyo ilikua imefungwa.

Binti aliyekuwepo katika mgahawa huo alianza kupiga kelele akidhani kavamiwa na mwizi. Mlinzi wa eneo hilo (mmasai) alimvaa kijana huyo na kumshambulia.

Baada ya tukio hilo taarifa zinasema walitokea watu wawili waliojitambulisha kuwa ni askari; askari hao walizuia watu waliozidi kujitokeza katika eneo hilo kuendelea kumpiga kijana huyo.

Wakiwa njiani, wananchi hao waliokuwa wakifuatilia kama atafikishwa kituo cha Polisi waliona wanachalewa na kuamua kuchukua sheria mkononi kwa kuendelea kumpiga kabla ya kumchoma moto.
chanzo: http://frankleonard.blogspot.com

No comments:

Post a Comment