STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 3, 2014

Domayo nje Azam kwa miezi minne kisa upasuaji

MABINGWA wa soka nchini, Azam Fc, imesema kiungo wake Frank Domayo atakuwa nje ya uwanja wa muda wa miezi minne kufuatia upasuaji wa mguu aliofanyiwa nchini Afrika Kusini.
Akizungumzia jiji Afisa Habari wa Azam, Jaffar Idd  amesema uchunguzi wa afya wa kiungo huyo aliofanyiwa na mganga mkuu wa klabu hiyo Dk Mwamkemwa ulibaini kuwa Domayo ana matatizo ya msuli wa mguu wake wa kushoto na kwamba atatakiwa kufanyiwa upasuaji.
Domayo alipekwa na uongozi wa Azam wiki iliyopita nchini Afrika Kusini akiambatana na Dk Mwankemwa ambapo juzi alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Vicent Parent na imeelezwa kuwa anaendelea vizuri huku akitarajiwa kurejea nchini Jumapili.
  Afisa Habari huyio amesema kiungo huyo atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi miezi minne akiendelea kupata tiba na uangalizi wa karibu wa jeraha lake kabla ya kurejea uwanjani kuitumikia klabu yake hiyo mpya ambayo amejiunga nayo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment