STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 26, 2012

Manchester City hoi Kombe la Ligi, Chelsea yaua

Wachezaji wa Man City wakiwa hoi baada ya kujifunga moja ya mabao yaliyoizamisha jana mbele ya Aston Villa

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, imeanza vibaya msimu kwa kung'olewa   mapema kwenye michuano ya Kombe la Ligi baada ya kulazwa mabao 4-2 na Aston Villa, huku vinara wa ligi hiyo ya England, Chelsea ikitoa kichapo cha  mabao 6-0 kwa 'Mbweha'.
Kipigo hicho toka kwa Aston Villa, kimempa wakati mgumu kocha wa Man City, Roberto Mancini, kwani ni dalili za kushindwa kurejea mafanikio iliyopata msimu uliopita ilipotwaa taji la Ligi Kuu baada ya miaka 50.
Matokeo mengine ya mechi za jana za michuano hiyo ya Kombe la Ligi ni kama ifuatavyo;
Bradford iliinyuka Burton Abilion mabao 3-2 katika muda wa nyongeza, Chelsea  ilivuna ushindi wa mabao 6-0 kw Wolves, Crawley ilinyukwa mabao 3-2 na Swansea, Leeds United ikainyoa Everton magoli 2-1.


Wachezaji wa Chelsea wakishangilia moja ya mabao yao katika mechi ya Kombe la Ligi jana usiku
Mechi nyingine Manchester City vs Aston Villa baada ya muda wa nyongeza 2-4,MK Dons ikalala mabao 2-0 kwa Sunderland, Preston iliangukia pua mbele ya Middlesbrough kwa kichapo cha mabao 3-1 na Southmpton ilivuna ushindi wa mabao 2-0 kwa Sheffied Wed, Swindon iliinyuka Burnley 3-1 na wagonga nyundo wa West Ham wakalala mabao 4-1 kwa Wigan.

No comments:

Post a Comment