STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 13, 2013

GOLDEN BUSH VETERANI WALIVYOISASAMBUA WAHENGA FC JANA

Mlezi wa timu ya Goldoen Bush Veterani, Onesmo Waziri 'Ticotico' akihojiwa na waandishi wa habari katika mchezo wao na Wahenga Fc ambapo timu yao ilishinda mabao 4-3.

Mshambuliaji Herry Morris akitafakari wakati wa mapumziki, ambapo alishatupia mabao mawili na kuisaidia Golden Bush kushinda mabao 4-3.

Wachezaji wa Golden Bush Veterani wakiwa mapumziko


Herry Morris akihojiwa na waandishi

Beki wa timu ya Golden Bush, Majaliwa 'Afande' akijohiwa pia kwenye mchezo huo

Yona Babadimo wa Wahenga Fc naye akihojiwa wakati timu yake ikichezea kipigo toka kwa Golden Bush jana jijini Dar es Salaam waliposherehekea Mapinduzi na kuukaribisha mwaka 2013


Mengi Matunda mchezaji wa Wahenga akijohiwa baada ya kupumzishwa na benchi lake la ufundi

Said Swedi 'Panucci' akikokota mpira katika pambano lao la jana

Njoo sasa! Ndivyo anayoelekea kusema beki wa Wahenga 'Mohammed huku Godfrey Katepa wa Golden Bush akimfuata

Achia wewe! Said Swedi (3) akichunana na mchezaji wa Wahenga katika pambano lao la jana

Kama Ronaldo! Mchezaji wa Wahenga akijiandaa kupiga mpira huku Shaaban Kisiga (19) wa Golden Bush akimfuatilia sambamba na wachezaji wenzake

Mimi ndio Macocha! Macocha Mayay wa Wahenga akimtoka Godfrey Katepa (kulia) huku akichungwa na Salum Swedi 'Kussi' wa Golden Bush Veterani.

Wachezaji wa Wahenga na Golden Bush wakiwajibika uwanjani timu zao zilipokutana jana na Golden Bush kushinda mabao 4-3

Macocha wa Wahenga Fc akijaribu kutafuta mbinu za kumtoka Saidi Swedi wa Golden Bush

Mzee Hamis wa Wahenga akikokota mpira pembeni ya uwanja wa TP wakati timu yake ilipoumana na Golden Bush na kuchezea kichapo cha mabao 4-3

Wazir Mahadhi (10) akichuana na wachezaji wa Wahenga wakati akiiongoza timu yake kulipa kisasi cha mabao 4-3 kwa wapinzani wao.

Pilikapilika uwanjani wakati Wahenga Fc na Golden Bush zilipomenyana jana jijini Dar es Salaam

Onesmo Waziri 'Ticotico' (4) akipongezwa na Athuman Machupa wakati wakimpisha uwanjani jana katika pambano lao dhidi ya Wahenga Fc.

Jamani Mpo Wapi! Beki wa Wahenga Fc akijiandaa kupiga mpira mbele

Mahadhi akichuana na mchezaji wa Wahenga katika mechi ya jana

Said Swedi 'Panucci' (3) akitafakari namna ya kuupiga mpira wakati wa pambano lao la Golden Bush dhidi ya Wahenga ambapo walifanikiwa kushinda mabao 4-3

Macocha Mayay wa Wahenga (kulia) akiwatoka wachezaji wa Golden Bush, Shaaban Kisiga (kushoto) na Shija Katina (8)

Berki wa Wahenga Fc akihamisha mpira mbele ya Herry Morris (kulia)

Hapa Kazi Tu!

MTANIKOMA! Macocha akiwaacha wachezaji wa Golden Bush katika pambano la jana, mchezaji huyu ndiye aliyekuwa nyota kwa upande wa Wahenga, japo timu yake ililala kwa mabao 4-3


Jamani eeh inakuwaje magoli yamerudi? Ndivyo anavyoelekea kuhoji kocha Madaraka Seleman wa Golden Bush wakati wa mapumziko ambapo timu yake ilikuwa imefungana mabao 2-2 na Wahenga Fc licha ya wao kuongoza kwa mabao 2-0. Waliporejea uwanjani kwa ngwe ya pili walirekebisha makosa na kuisambaratisha Wahenga kwa magoli 4-3

MTANIJUA LEO! Nyota wa Wahenga Macocha Mayay akiwakimbiza wachezaji wa Golden Bush, Godfrey Katepa (9) na Majaliwa (14) wakati timu zao zilipomenyana jana kwenye mechi maalum ya kuukaribisha mwaka 2013 na kusherehekea sikukuu ya Mapinduzi. Golden Bush ilifanikisha kushinda mabao 4-3

No comments:

Post a Comment