STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 15, 2013

Zola D, P Funk wote wana Knockout

Msanii Zola D akiwa katika pozi


MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, David Michael 'Zola D' ameuanza mwaka 2013 kwa  kishindo kwa kuachia wimbo wake mpya uitwao 'Knockout' aliomshirikisha mtayarishaji mahiri wa muziki, P. Funk 'Majani'.
Tayari wimbo huo uliotolewa katika 'audio' na video tayari umeshaanza kurushwa hewani katika vituo vya redio na runinga nchini, huku Zola D akidai hizo ni salamu zake kwa mashabiki kwamba mwaka 2013 amejipanga kuwapa raha mwanzo mwisho.
Zola D alisema kuwa, wimbo huo ameurekodia studio za Bongo Rocords kwa Majani na video ameifanya chini ya kampuni yake ya Uncle Films akishirikiana na kampuni ya Benjamini wa Mambo Jambo.
"Katika kuwapa raha mashabiki wangu, nimeachia hewani wimbo wangu mpya uitwao 'Knockout' ambao nimeimba na P Funk 'Majani' ambayo pia nimeitolea video yake na tayari imeshaanza kuchezwa na vituo vya redio na runinga," alisema Zola D.
Mkali huyo ambaye pia ni mwanamasumbwi wa uzito wa juu nchini, alisema wakati wimbo huo ukiendelea kutamba hewani, ameshaanza maandalizi ya kufyatua kazi nyingine mpya, japo hakupenda kuweka hadharani kwa madai ni mapema mno.
"Ndugu yangu unajua siku hizi wasanii wamekuwa wepesi kuiba 'idea' za wenzao, hivyo kutaja jina la 'project' yangu mpya ijayo inaweza kuwa mtaji kwa wachakachuaji, ila mashabiki wakae wakijua kuna burudani mpya nawaandalia," alisema Zola D.
Msanii huyo alisema kazi hiyo mpya huenda ikakamilika ndani ya wiki ijayo kabla ya kufanyiwa utaratibu ya kuachiwa hewani baada ya kukamilika kila kitu ikiwemo kurekodiwa kwa video yake.

No comments:

Post a Comment