STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 15, 2013

Extra Bongo waja na Wiki 4 za Kutoa Zawadi kwa Mashabiki

Mkurugenzi wa Extra Bongo Ally Choki akiwapagawisha mashabiki wa bendi hiyo katika moja ya maonyesho yao
BENDI ya dansi inayotisha nchini kwa sasa, Extra Bongo 'Wana Next Level' a.k.a Wazee wa Kizigo imeandaa wiki nne za kuwazawadiwa mashabiki wake katika shindano maalum litakalofahamika kwa jina la 'Wiki 4 za Zawadi za Extra Bongo'.
Shindano hilo litakaloshindanisha mashabiki wa bendi hiyo kwa kunengua miondoko ya bendi hiyo ya 'Kizigo' ndani ya wiki nne mfululizo ambapo kwa kuanzia watatoa zawadi hizo kwenye ukumbi wa Meeda Club, Sinza jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki alisema katika shindano hilo mashabiki watatu watakacheza vema muziki wa bendi hiyo watawazadiwa vitita vya fedha taslim ukumbini.
Choki alisema mshindi wa kwanza katika shindano hilo lililoandaliwa kwa nia ya kuongeza hamasa kwa mashabiki wao kupima kama nao ni wakali wa muziki atapewa Sh 150,000 wakati wa pili atazawadiwa Sh 100,000 na wa tatu ataambulia Sh 50,000.
"Extra Bongoi tunatarajia kuja na Wiki Nne ya Zawadi kwa Mashabiki ambayo rasmi itaanza Jumamosi kwenye ukumbi wa Meeda Club, Sinza kabla ya kuelekea TMK Ijumaa ya Januari 25 ksiha kuangalia kama tuhamie Bagamoyo au Kibaha," alisema Choki.
Choki alisema uzinduzi rasmi wa shindano hilo utasindikizwa na wakali wa muziki wa kizazi kipya, Amin, Linah na Ditto kutoka THT na Saynag wa Respect.
"Yaani ni burudani kwa kwenda mbele pamoja na kuwashuhudia mashabiki wakichuana kucheza Kizigo, pia watawashuhudia wakali wa muziki wa kizazi kipya ambao watatusindikiza katika wiki hizo nne za kutoa zawadi kwa mashabiki wetu," alisema.
Choki alisema japo mpambano huo wa mashabiki sio shindano haswa kwa sababu halitakuwa na majaji wala waamuzi, zaidi ya mashabiki lakini wamefanya hivyo ili kuonyesha namna gani wanavyowathamini mashabiki wao waliowaunga mkono karibu miaka mitatu ya kurejea kwao upya katika 'game'.

No comments:

Post a Comment