STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 15, 2013

ZAWADI ZA EXTRA BONGO KUANZA KUTOLEWA MEEDA CLUB

Ally Choki na Athanas Montanabe wakiwajibika jukwaani

MASHABIKI wa bendi ya Extra Bongo wanatarajiwa kuanza kuzoa zawadi katika shindano lao maalum lililopewa jina la 'Wiki 4 za Zawadi Extra Bongo' siku ya Jumamosi katika onyesho litakalofanyika kwenye ukumbi wa Meeda Club, Sinza Mori, Dar es Salaam.
Shabiki atakaayecheza vema katika onyesho hilo atazoa kitita cha Sh Laki Unusu (150,000) huku wa pili akizoa Laki Moja (100,000) na wa tatu yeye ataambulia Nusu Laki (50,000).
Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki alisema utaratibu huo wa kutioa zawadi hizo kwa mashabiki wao utafanyika katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya jijini Dar es Salaam kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia Januari 19.
Choki alisema mara watakapotoka Meeda Extra Bongo watapeleka zawadi kwa mashabiki wao wa Temeke kabla ya kuelekea Kibaha Pwani na mahali pengine watakapoona panafaa kwenda kumwaga zawadi hizo kama njia ya kurudisha shukrani kwa mashabiki wao waliowaunga mkono tangu bendi hiyo irejee upya 2010.
"Tunataka mashabiki wafurahie burudani na pia kuondoka ukumbini wakiwa na zawadi kama ambavyo walivyokuwa wanatuunga mkono tangu tuliporejea kwa awamu ya pili na sasa tukielekea miaka mitatu," alisema.
Choki alisema kila watakapokuwa wakikaribia kumaliza onyesho watawapigia sebene mashabiki wao na kuchuana wenyewe na watawapa fursa mashabiki watazamaji kuteua washindi ambao watapewa chao hapo hapo kabla ya kuelekea mahali pengine hadi watakaporidhika na kusitisha mchuano huo.
Naye kiongozi wa safu ya uenguaji ya Extra Bongo, Hassani Mussa 'Syper Nyamwela' alisema anadhani mchuano huo ni fursa nzuri ya mashabiki wao kuifurahia Extra Bongo sambamba na kutunisha mifuko yao kwa kuonyesha umahiri wao wa kucheza miondoko ya bendi hiyo.
"Badala ya kutozoea kwa muda mrefu kutuona wanenguaji na wana Extra Bongo kwa ujumla kuonyesha umahiri wa kunengua safari hii ni zamu yao kushindana wenyewe kwa wenyewe na kuzoa fedha taslim bila zengwe wala nini, na huu ni mwanzo tu tutarejesha fadhila kwa mashabiki kadri tutakavyojipanga," alisema.

Bendi hiyo ya Extra Bongo inayotamba na vibao matata kama 'Ufisadi wa Mapenzi', 'Mjini Mipango', 'Mgeni' na nyingine, itakuwa bendi ya kwanza kwa mwaka huu na siku za karibuni kufanya kitu kama hicho ili kuwafurahisha mashabiki ambao wamekuwa wakiwaunga mkono kwa kuhudhuria maonyesho wao kila mahali.

No comments:

Post a Comment