STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 24, 2013

Zola D ana Swahili Hip Hop


Zola D katika pozi
MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, David Mlope 'Zola D' anajiandaa kupakua albamu yake ya kwanza tangu atuimbukie kwenye fani hiyo itakayokuwa na nyimbo 21.
Akizungumza na MICHARAZO, Zola D, alisema albamu hiyo itafahamikwa kwa jina la 'Swahili Hip Hop' ambayo imekusanya nyimbo zake zote alizozifyatua tangu aingie kwenye fani hjiyo mwaka 1995.
Zola D alisema, baadhi ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo ni pamoja na kibao kilichompa ujiko miaka kadhaa iliyopita cha 'Moto wa Tipper', 'Jana Sio Leo', 'Sipati Mchongo', 'What Going On', 'Hustler King', 'Unde', 'Msela Sana', Rap Gangster' na 'Rudi'.
Nyingine ni nyimbo zake mbili za hivi karibuni ambazo zinaendelea kutamba katika vituo vya redio na runinga za 'Coast to Coast' na 'Knockout' alioimba na P Funk.
"Nimeshakamilisha kila kitu kabla ya kuitoa hadharani albamu yangu itakayokuwa ya kwanza tangu nitumbukie katika fani hii miaka karibu 20 iliyopita, itakuwa na nyimbo za zamani na mpya ambazo baadhi zinaendelea kutamba nchini na nje ya nchi," alisema.
Msanii huyo ambaye pia ni bondia wa ngumi za kulipwa wa uzito wa juu akiwa pia amesilimu kutoka dini ya Ukristo akifahamika kwa jina la Daud, alisema mashabiki wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiuulizia juu ya albamu hiyo waondoe shaka.

No comments:

Post a Comment