STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 27, 2014

Inspekta Harun kutambulisha mpya, akisdaka mrembo Mbeya

Inspekta Harun 'Babu' katika pozi
MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Haruna Kahena 'Inspekta Harun' a.k.a Babu anatarajiwa kuitambulisha albamu yake mpya ya 'Sharubu za Babu' sambamba na video ya wimbo wake wa 'Hujachelewa' jijini Mbeya wikiendi hii.
Akizungumza na MICHARAZO, Inspekta alisema kuwa, utambulisho huo utafanyika siku ya Jumapili kwenye ukumbi maarufu jijini humo ambao utaambatana pia na shindano la kusaka kimwana wa kucheza filamu ya 'Mtoto wa geti Kali'.
Staa huyo wa nyimbo kama 'Nje Ndani', 'Simulizi la Ufasaha', 'Mtoto wa Geti Kali' na nyingine, alisema shindano hilo la kusaka mrembo wa kucheza filamu hiyo ya Mtoto wa Geti Kali utafanyika kila mahali atakapoenda kutambulisha albamu na video hiyo.
Alisema mwishoni watakaopatikana watashindanishwa kwa pamoja ili kupata kisura mmoja ambaye ndiye atakayekuwa mhusika mkuu wa filamu hiyo ambayo inatokana na wimbo wake uliowahi kutamba miaka ya nyuma wenyue jina hilo.
"Natarajia kuzindua video ya wimbo wangu mpya wa 'Hujachelewa' sambamba na kutambulisha albamu ya 'Sharubu za Babu'," alisema na kuongeza;
"Onyesho hilo litafanyika Machi 2, jijini Mbeya na litaenda sambamba na shindano la kusaka mrembo wa kucheza filamu yangu ya Mtoto wa Geti Kali na nitasindikizwa na wasanii kadhaa nyota wa jijini humo na wale wa Dar," alisema Inspekta Harun.
Msanii huyo alisema orodha ya watakaomsindikiza anatarajiwa kutangaza kesho ili kuwaweka tayari mashabiki wake kuwapokea vyema katika onyesho hilo la Jumapili.

No comments:

Post a Comment