STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 3, 2013

Mfanyabiashara Kariakoo ajirusha toka ghorofa ya 9, kisa...

Mfanyabiashara huyo akiwa hoi kando ya gari alilolidondokea ambalo liliharibika vibaya kama inavyoonekana pichani
MCHANA wa leo mitaa ya Kariakoo, mtu mmoja aliyetambulika kwa jina moja tu la Shirima,  ambaye anadaiwa ni mfanyabiashara katika moja ya maduka yaliyopo eneo hilo la  Kariakoo, Dar es Salaam, amejirusha toka ghorofa ya 9 ya Hoteli ya Concord.
habari ambazo zimepatikana na kusimuliwa na mashuhuda wa tukio hilo lililosikitisha wengi, linasema kuwa mfanyabiashara huyo alijirusha toka kwenye jengo hilo na kuangukia gari kabla ya kukimbizwa hospitali kwa uangalizi zaidi maana haijafahamika kama kapoteza Maisha au bado yu hai.

Mfanyabiashara huyo alijirusha toka ghorofani na kuangukia Gari aina ya Toyota Corolla ambayo ni taxi iliyokuwa imepaki nje ya hoteli hiyo....chanzo cha kujirusha kwa mfanyabiashara huyo bado hakijafahamika mpaka sasa.

Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea muda si mrefu wanaeleza kuwa walipatwa na mshuko baada ya kusikika kishindo cha kitu kilichokuwa kimeangukia gari hilo na waliposogea kushuhudia ndipo walipobaini kuwa alikuwa ni mtu huyo alietambulika kwa jina moja la Shirima.

No comments:

Post a Comment