STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 10, 2012

Mbunge Vicky Kamata amwaga misaada kwa walemavu, yatima mkoani Geita







MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa Mpya wa Geita, Vicky Kamata, amemwaga msaada wa wenye thamani zaidi ya Sh Milioni 10, unaohusisha vyakula, mavazi, magodoro na viti vya walemavu (wheel chair) 30 kwa wakazi wa tarafa ya Bugando mkoani humo.
Misaada hiyo ambao ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake kwa wakazi wa Geita waliomsaidia kuchaguliwa kwake kuwa mbunge kupitia CCM, ulitolewa juzi katika tarafa hiyo na vituo vya kulelea na kutunzia yatima vya Lelea na Feed & Tend International.
Kwa mujibu wa Kamata, misaada hiyo imehusisha viti vya walemavu 30, magodoro 50, maziwa, vyakula na nguo vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 10 na kudai ugawaji huo umefanyika kwa awamu ya kwanza na utaendela kwa awamu nyingine mbili.
"Hii ni awamu ya kwanza ya utekelezaji wa ahadi zangu kwa wakazi wa Geita katika kuwasaidia wenye matatizo, natarajia kuendelea na ugawaji kama huo utakaohusisha baiskeli nyingine 50, ambazo tayari zimeshawasili toka nje ya nchi," alisema Kamata.
Mbunge huyo kijana, alisema misaada hiyo na mingine ambayo amekuwa akitoa kwa watu wenye matatizo mkoani mwake inafanywa chini ya mfuko wake wa Victoria Foundation ambayo yeye ni Mwenyekiti wake ikishirikiana na wafadhili wa nje ya nchi.
Alisema ukiondoa utekelezaji wa ahadi zake, lakini misaada hiyo inalenga kuwasaidia watu wenye matatizo waliopo mkoani humo, wanaondokana na adha walizonazo na kufurahia maisha kama watu wengine.

Mwisho

No comments:

Post a Comment