STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 28, 2014

Neymar, Muiller, Messi wabanana kuwania kiatu cha Dhahabu

Neymar wa Brazil
Lionel Messi wa Argentina
Thomas Muiller wa Ujerumani  
WAKATI  kinyang'anyiro cha hatua ya mtoano ya 16 Bora ikianza rasmi leo kwa michezo miwili itakayozikutanisha timu za Amerika Kusini, hatua ya makundi ya Fainali za Kombe laDunia 2014 imevunja rekodi.
Jumla ya mabao 136 yamefungwa katika hatua hiyo, sita zaidi ya yale yaliyofungwa katika fainali za 2002.
Wachezaji watatu, Lionel Messi wa Argentina, Neymar wa Brazil na Thomas Muiller wa Ujerumani wanachuana kileleni katika orodha ya wafungaji bora.
Kila moja kati ya wachezaji hao amefunga mabao manne wakifuatiwa na wachezaji sita wenye mabao matatu kila mmoja.
Neymar ana nafasi ya kuongeza idadi ya mabao yake kama leo ataendelea kucheka kwenye mechi yao na Chile kuwania kufuzu Robo Fainali.
Messi atakuwa na nafasi ya kuendelea kunguruma wakati atakapoiongoza Argentina kuvaana na Uswisi siku ya Jumatatu katika mechi nyingine ya 16 Bora.
Ukiondoa wakati hao wenye mabao manne, wachezaji wenye magoli matatu kila mmoja ni pamoja na Robin van Persie, Arjen Robben wote wa Uholanzi, Karim Benzema wa Ufaransa, Enner Valencia wa Ecuador, James Rodriguez wa Colombia na Xherdan Shaqiri wa Uswisi.
Kati ya hapo ni Valencia tu ndiye hana nafasi ya kuongeza idadi yake ya mabao kwa vile timu yake imeshaaga michuano hiyo nchini Brazili.
Katika orodha ya wafumania nyavu hiyo pia wapo wachezaji wenye mabao mawili mawili ambao ni;Tim Cahill wa Australia, Mario Mandzukic wa Croatia, Martinez wa Colombia, Dempsey wa Marekani, Wilfried Bony wa Ivory Coast, Andre Ayew wa Ghana, Asamoah Gyan wa Ghana, Ahmad Mussa wa Nigeria na Slimani wa Algeria.
Ukimuondoa Dempey wa Marekani, Mussa wa Nigeria na Slimani wa Algeria waliosalia timu zaoi zimeshaaga michuano na hivyo hawana nafasi ya kuongeza idadi.

No comments:

Post a Comment