STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 28, 2014

Liverpool sasa kumuua Suarez kuwabeba Lallana na Markovic

Suarez akiwajibika siku ya mechi dhidi ya England kabla ya kuja kuharibu wakiumana na Italia
KLABU ya soka ya Liverpool ipo kwenye mpango wa kumuuza nyota wake Luis Suarez katika klabu ya Barcelona, ili kupata fedha za kuwanyakua Adam Lallana na Lazar Markovic.
Barcelona imetajwa kuoingoza mbio za kumnyakua mchezaji huyo aliyefungiwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) baada ya kumng'ata beki wa Italia Giorgio Chiellini .
Klabu hiyo ya Hispania imeweka wazi kuwa hata kama Suarez amefungiwa miezi minne kucheza soka, hiyo haizuii nia yao ya kumsajili na mpaka sasa Liverpool hawajahangaika kutafuta mbadala wa mshambuliaji huyo hatari.
Ingawa Liverpool walikuwa wanaweka ngumu kwa dau hilo, lakini baada ya kupokea taarifa za FIFA kuhusu kumfungia Suarez wamelazimika kukubali na kumruhusu Muurguay huyo kuondoka klabuni hapo.
Licha ya kufungiwa, Liverool wanaamini Barcelona inaweza kulipa paundi milioni 80 na tayari mmiliki mkuu wa klabu hiyo John W Henry anaonekana kutokuwa tayari kumuuza kwa bei rahisi.
Mwanasheria wa Suarez Alejandro Balbi alikuwa Barcelona kujadili hatima ya mteja wake, wakati kocha mpya wa Barca Luis Enrique alisema hakuna tatizo lolote juu ya kumsajili nyota huyo mwenye miaka 27.
Alimfananisha Suarez na mshambuliaji gwiji wa Barca Hristo Stoichkov na alisema : ‘Stoichkov kiukweli aliwahi kufanya madhambi makubwa dhidi ya mwamuzi, lakini aliendelea kufirika kuwa mcheza mkubwa".
Kama Liverpool watamuuza Suarez kwa paundi milioni 80, hiyo itakuwa biashara nzuri kwa Brendan Rodgers ambapo atatumia mkwanja huo kuimarisha kikosi chake.
Wachezaji ambao Liverpool inawapigia jaramba kuwanasa ni Adam Lallana kutoka Southampton anayetajwa atakuwa mali ya Vijogoo hao wekundu  saa 24 zijazo baada ya Southampton kukubali ofa ya paundi milion 25 kwa mshambuliaji huyo wa England, na hii ni baada ya kupita wiki nne tangu apokee simu kutoka kwa maofisa wa Anfield ambao pia wameanza mbio za kumuwania mchezaji wa Benfica, Lazar Markovic.
Mserbia, Markovic ni moja ya wachezaji bora wenye umri mdogo katika soka la Ulaya na bei yake ni paundi milioni 20.

No comments:

Post a Comment