STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 28, 2014

Mashetani Wekundiu wazidi kujiimarisha England

Jembe Jipya! Luke Shaw akiwa na jezi mpya ya klabu yake ya Manchester United
Ander Herrera alipotangazwa ramsi kujiunga kwa Mashetani Wekundu
MABINGWA wa zamani wa England, Manchester United imezidi kuimarisha kikosi chake baada ya kufanikiwa kumsainisha beki wa kushoto wa Southamptom na timu ya taifa ya nchi hiyo iliyotolewa kwenye Kombe la Dunia, Luke Shaw.
Kwa mujibu wa duru za kandanda za England zinasema kuwa, Mashetani Wekundu hao wamekamilisha uhamisho wa Shaw kwa gharama za Pauni Milioni 31.5 kwa mkataba wa miaka minne.rd.
Mchezaji huyo amekamilisha vizuri vipimo afya katika Uwanja wa mazoezi wa United, Carrington na ameambiwa atakuwa beki wa kushoto chaguo la kwanza la kocha Louis van Gaal.
Inafahamika amehakikishiwa namba na beki mkongwe mwenye umri wa miaka 33, Patrice Evra, ambaye atabakia United, anatarajiwa kupunguziwa majukumu klabuni hapo. 
Usajili wa Shaw umekuja siku moja baada ya klabu hiyo kufanikiwa kunyakua Ander Herrera kutoka Athletic Bilbao kwa ofa ya pauni milioni 29.
Man United ilikuwa na msimu mbaya ligi iliyopita chini ya kocha David Moyes ambaye alitimuliwa na nafasi yake kushikiliwa kwa muda Ryan Giggs kabla ya Luis van Gaal kupewa kibarua cha kuwa kocha mkuu sasa.

No comments:

Post a Comment