STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Golden Bush Veterani, Wahenga kesho hapatoshi Kinesi

Onesmo Waziri 'Tictico'
PAMBANO la kirafiki la kusherehekea sikukuu ya Pasaka kati ya Golden Bush Veterani na wapinzani wao wakuu, Wahenga Fc limehamishiwa uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Awali pambano hilo lilipangwa kufanyika kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza, lakini kutokana na mvua zinazoendelea jijini Dar zimeufanya uwanja huo kujaa maji na hivyo kutofaa kutuchezeka.
Mlezi na Msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema muda wa kuanza pambano hilo ni ule ule wa saa 10 jioni japo wamebadili uwanja.
"Napenda kutoa taarifa kwamba ile game yetu ya kesho imehamishiwa uwanja wa Kinesi, hii imetokana na hali ya mvua iliyoharibu kabisa uwanja wetu wa TP maarufu kama Nangwanda Sijaona. Game itaanza muda uleule wa saa kumi na nusu jioni.
Ticotico alisema kikosi chao kimejiandaa vya kutosha kuweza kula Pasaka vyema kwa kuilaza Wahenga Fc.





No comments:

Post a Comment