STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 31, 2013

GOLDEN BUSH VETERANI YAIZAMISHA WAHENGA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigEXcYZjHBYFe7oOEgW5OFabOhx7fWDF32Rsh1DNIyJgIuc8Evl-_yJ_6-t3SWerT20D7radHa4TQSZKy32dCj_g7jev9QWI1KeveOocs9OaXA0c4U8BREl7bBYDCuQ4pz95KuTxPJFBI/s1600/Golden+Bush+Veterani.JPG
Kikosi cha Golden Bush Veterani
 
WAKALI wa soka la maveterani jijini Golden Bush Veterani jioni ya leo imeisherehekea vyema sikukuu ya Pasaka baada ya kuwafumua wapinzani wao wakuu, Wahenga Fc kwa kuwalaza mabao 2-1 katika pambano maalum lililochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo Dar es Salaam.
Mchezo huo uliochezwa huku mvua kubwa ikinyesha na kuhudhuriwa na Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye ulishuhudiwa Wahenga wakitangulia kupata baop la kuongoza lililotumbukizwa wavuni na Albert Shao.
Hata hivyo Golden Bush iliyokuwa ikiongozwa na nahodha wake, Onesmo Wazir 'Ticotico' ilisawazisha bao hilo kupitia kwa nyota wa pambano hilo, Sadick Muhimbo na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe nguvu sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji ambapo iliongeza uhai wa pambano hilo ambalo pande zote zilionyesha kulikamia na kuhiotaji ushindi ili kulinda heshima mbele ya mwenzake, japo utelezi na maji yaliyosababishwa na mvua iliyokuwa ikinyesha ilipunguza utamu wa soka la timu hizo.
Golden Bush ilifanikiwa kuandika bao la pili la la ushindi kupitia kwa 'Super Sub' wao De Natale alifumua shuti kali baada ya mabeki wa Wahenga kuzembea kuokoa mpira langoni mwake.
Mpaka filimbi ya mwisho ya mwamuzi wa pambano hilo, Ally Mayay ilipolia kuashiria pambano hilo limemalizika Wahenga walijikuta hoi kwa wapinzani wao kwa kula kichapo cha mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment