STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 29, 2013

BREAKING NEWSSSS: GHOROFA LAPOROMOKA DAR 60 wadaiwa kufukiwa


HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema jengo la ghorofa lililokuwa likiendelea kujengwa mitaa ya Indra Gandi jijini Dar es Salaam limeporomoka na kuwafukia watu wasiopungua 60.
MICHARAZO imedokezwa kuwa mpaka sasa watu 17 wameshaokolewa na miili ya watu wawili imepatikana katika mkasa huo unaohusisha ghorofa hilo la orofa 19.
Mtandao unaendelea kuzifuatilia taarifa hizo kisha tutawajulisha kinachoendelea, japo inaeleza juhudi za uokozi katika tukio hilo zinaendelea kunusu watu waliozikwa na kifusi cha jengo hilo.
Pia imeelezwa kuwa viongozi wa mkoa akiwemo Rc Mecky Sadick ametua katika eneo hilo akiambatana na wenzake kwa ajili ya kujua kinachoendelea. 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova amethibitisha kuokolewa kwa watu 17 na wawili kupoteza maisha na kusema taarifa kamili itatolewa baadaye.

No comments:

Post a Comment