STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 28, 2014

Kama Ustaadh, mcheki Cristiano Ronaldo katika vazi takatifu


Cristiano Ronaldo akiwa kwenye mavazi ya kiislam akipiga picha na mashabiki huko Dubai.

NYOTA wa klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo alionekana na kupigwa picha na mapaparazi kwenye matembezi yake binafsi Dubai akiwa amevalia mavazi ya Kiislam na yaliompendeza sana.

Cristiano Ronaldo ambaye yeye si Muislam, alionekana kupendeza kupita kiasi katika vazi hilona alidai alipendezwa na uvaaji huo baada ya kuina watu wengi waishio Dubai katika vazi hilo kuu na kujihoji vipi naye asiwe miongoni mwa waliovaa vazi hilo. 
Pia hakuwahi kuvaa vazi la dini hiyo alionelea avae kwa ishara ya kuiheshimu dini hiyo na kuona sio kitu kibaya kuwa miongoni kwao kimavazi.

Cristiano Ronaldo akiwa kwenye vazi jingine la kiislamu huko Dubai

Mchezaji huyo alikuwa Dubai wiki iliyopita kwenye mapumziko yake binafsi mbali na shughuli za kimpira. Alienda kutembea huko kabla ya wiki ya sikukuu za Krismasi sambamba na mwanae aliyemvisha pia vazi hilo la kanzu.
Alionekana ni mwenye kufurahishwa na mandhali ya mji huo pia utamaduni wao wa chakula pia kimavazi ndio mana nae alipendezwa kuvaa kama wao.

Vazi lingine alilovaa mchezaji Cristiano Ronaldo akiwa kwenye matembezi yake binafsi Dubai.

Mchezaji huyo alikaa Dubai kwa siku nne wiki iliyopita na baadae aliondoka kurejea Hispania ambapo alijiunga na wachezaji wenzake kwenye kambi ya maandalizi ya mechi zilizoendelea katika ligi ya nchi hiyo anakochezea.

No comments:

Post a Comment