STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 30, 2014

BABY MADAHA ANAKUJA NA SAINT & GHOST

http://api.ning.com/files/KtF8hZpsH-3lMXDW7ufVoIr4iNPkkwwMRNxku*jb0MDMU7Iz*sLL7Hfl9BdoYxrd9FpJEMbPW8DsGjHTHEQX05k1rl-IZhsZ/babymadaha.jpg
Baby Madaha
BAADA ya kutuymia muda mrefu akiwa amejichimbia Kenya kufanya shughuli zake za muziki, mwanadada Baby Madaha anajiandaa kuvunja ukimya kwenye soko la filamu kwa kuibuka na 'Saint & Ghost'  ambayo imesheheni nyota mbalimbali wa filamu nchini.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo, Baby Madaha alisema filamu hiyo inayotengenezwa kupitia kampuni yake, iitwayo Darkangel Film Production and Entertainment imewashirikisha wakali kama Kulwa Kikumba 'Dude', yeye (Baby Madaha), Hidaya Njaidi,  Grace Mapunda 'Mama Kawele', Ramadhani Ally 'Tafu', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo' na wengine.
"Nimbo chimbo kwa sasa natengeneza filamu yangu iitwayo 'Saint and Ghost' ambayo naitengeneza kupitia kampuni yangu na inawashirikisha wasanii mbalimbali nyota nikiwamo mimi mwenyewe, Mzee Chillo, Mama Kawele, Mama Njaidi, Taffu, Dude na wengine na ni bonge la kazi la kuanzia mwaka 2015," alisema Baby Madaha.
Mwanadada huyo anayetamba na nyimbo kama 'Summer Holiday' akiwa na albamu mbili sokoni za Amore na Desperado' amejipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji wa filamu baadhi ya kazi alizowahi kuzicheza ni 'Nani', 'Misukosuko3', 'Mpishi', House Na.44' na 'Ray of Hope' iliyoshinda tuzo ya kimataifa nchini Nigeria.

No comments:

Post a Comment