STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 30, 2014

Liverpool yaendelea 'maajabu' EPL, yaifumua Swansea City 4-1

The 26-year-old is mobbed by his Liverpool team-mates after helping his side towards a vital three points at Anfield
Liverpool wakishangilia mabao yao
Moreno now has two Premier League goals to his name since joining Liverpool from Sevilla in the summer
Moreno akishangilia bao la kuongoza la Livwerpool
Reds midfielder Lallana runs towards the Kop in celebration of his second half goal
Adam Lallana akishangilia moja ya mabao yake mawili
Three Swansea players look on as Lallana sends a left-footed finish past Fabianski to send Liverpool into a commanding lead
Lallana akiwatesa mabeki wa Swansea
MABAO mawili yaliyofungwa na Adam Lallana na moja la kujifunga la beki wa Swansea City imeiwezesha Liverpool kupata ushindi wake wa pili mfululizo katika Ligi Kuu ya England.
Ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Anfield, Liverpool ilianza pambano hilo kwa mashambulizi langoni mwa wageni wao na kuandika bao la kwanza katika dakika ya 33 kupitia kwa Alberto Moreno aliyemalizia kazi ya Henderson.
Kipindi cha pili kilikuwa na mafanikio zaidi kwa vijana wa Branden Rodgers baada ya Lallana kuandika bao la pili dakika ya 51 kabla ya Swansea kuandikisha bao lao pekee dakika moja baadaye kupitia Gief Sigurdsson.
Adam Lallana alirudi tena kambani kwa kuandika bao la tatu la Liverpool dakika ya 61 na dakika tano baadaye beki wa Swansea City, Shelvey alijifunga katika harakati za kuokoa mpira na kuifanya Liverpool kupaata ushindi mnono wa mabao 4-1 na kuchupa hadi nafasi ya nane katika msimamo wa ligi hiyo.
Liverpool wamefikisha pointi 28 sawa na Swansea lakini imefanikiwa kuwashusha wapinzani wao kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ushindi huo wa Liverpool wa mabao manne ni wa kwanza tangu nyota wao, Lusi Suarez kutimkia Barcelona.

No comments:

Post a Comment