STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 30, 2014

DECEMBER LIKIZO FESTIVAL KUFANYIKA KESHO MBEZI BEACH

TAMASHA la tatu la December Likizo Festival linatarajiwa kufanyika kesho jijini Dar es Salaam likihusisha na maonyesho ya muziki, mavazi na filamu sambamba na semina mbalimbali juu ya kuboresha ufanisi wa vipaji vya sanaa.
Mratibu wa tamasha hilo, Steven Sandhu 'Triple S',  alisema kwa wiki nzima kumekuwa na shughuli mbalimbali za tamasha hilo na leo ndiyo kilele chake.
Sandhu ambaye ni mwanamitindo na muigizaji filamu alisema kilele cha tamasha (le grand Finale) la mwaka huu litafanyika kwenye hoteli ya Landmark iliyopo Mbezi Beach.
"Tamasha la tatu la 'December Likizo Festival kwa mwaka wa 2014 litafikia kilele kesho kwenye Landmark Hotel kwa maonyesho mbalimbali na kwa wiki nzima kuelekea kilele cga tamasha hilo kulikuwa na shughuli mbalimbali," alisema.
Sandhu alisema anashukuru uitikiaji wa wito kwa wasanii na washiriki wengine wa tamasha hilo na kuongeza imani yake kama ilivyokuwa kwa matamasha mawili ya nyuma ya mwaka 2012 na 2013, hata la mwaka 2014 litafana zaidi," alisema.

No comments:

Post a Comment