STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 25, 2014

Alex Song atemwa Cameroon kuelekea Afcon 2015

http://c.smimg.net/14/25/alex-song-cameroon.jpgKOCHA wa timu ya taifa ya Cameroon, Volke Finke ametaja kikosi cha awali cha wachezaji 27 kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta. 
Kocha huyo raia wa Ujerumani ameteua wachezaji wengi waliokuwemo katika mechi za kufuzu, lakini amemuacha kiungo Alex Song. 
Song hajaichezea Cameroon toka alipotolewa nje kwa kadi nyekundu katika kipindi cha mabao 4-0 walichopata kutoka kwa Croatia katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil. 
Kiwango kizuri alichokionyesha msimu huu akiwa kwa mkopo katika klabu ya West Ham United akitokea Barcelona, kilizua tetesi kuwa angeweza kuitwa katika timu ya taifa. 
Cameroon wanatarajiwa kuanza maandalizi nyumbani na watacheza mechi ya kirafiki na Congo Brazzaville Januari 7 kabla ya kusafiri kwenda Gabon kwa ajili ya kambi yao nyingine na kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini Januari 11.
Simba hao Wasiofugika wataanza kibarua chao katika michuano hiyo ya AFCON kama ratiba inavyoonesha hapo chini
20 Jan: v Mali in Malabo
24 Jan: v Guinea in Malabo
28 Jan: v Ivory Coast in Malabo
Kikosi kamili  kilichoteuliwa kabla ya kuchujwa baadaye ni hiki hapa;
Makipa: Joseph Ondoua (Barcelona, Spain), Guy Ndy Assembe (Nancy, France), Pierre Sylvain Abogo (Tonnerre Yaoundé)
Walinzi: Cédric Djeugoue (Coton Sport), Jérôme Guihi Ata (Valenciennes, France), Nicolas Nkoulou (Marseille, France), Ambroise Oyongo Bitolo (New York Red Bulls, USA), Brice Nlate Ekongolo (Marseille, France), Franck Bagnack (Barcelona, Spain), Henri Bedimo (Lyon, France),
Viungo: Stéphane Mbia (Seville, Spain), Enoh Eyong (Standard Liège, Belgium), Raoul Cedric Loe (CA Osasuna, Spain), Edgard Salli (Academica de Coimbra. Portugal), Georges Mandjeck (Kayseri Erciyesspor, Turkey), Franck Kom (Etoile du Sahel, Tunisia), Patrick Ekeng (FC Cordoba, Spain)
Washambuliaji: Eric-Maxim Choupo-Moting (Schalke 04, Germany), Benjamin Moukandjo (Reims, France), Jacques Zoua (Kayseri Erciyesspor, Turkey), Vincent Aboubakar (Porto, Portugal), Léonard Kwekeu (Caykur Rizespor, Turkey), Clinton N'Jie (Lyon, France), Franck Etoundi (Zurich, Switzerland)

No comments:

Post a Comment