STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 25, 2014

Nyota England anusurika kufa ajalini

MWENYEKITI wa zamani wa Chama cha Wachezaji wa Kulipwa nchini Uingereza, PFA, Clarke Carlisle, amenusurika kifo katika ajali mbaya ya barabarani iliyomfanya awahishwe hospitalini kwa kutumia ndege.
Jumatatu iliyopita Polisi walithibitisha kwa mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35 alikuwa amejeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na lori katika eneo la A64, karibu na Bishopthorpe York kiasi cha kuhitajika ndege ya dharura kumkimbiza hospitalini.
Hata hivyo vyombo vya habari vilivujisha kuwa aliyegongwa alikuwa ni Carlisle aliyesherehekea miaka 35 Oktoba mwaka huu na kwamba nyota huyo wa zamani wa England amelazwa Leeds General Infirmary kwa ajili ya matibabu zaidi.
Carlisle aliyewahi kuichezea timu mbalimbali zikiwamo za Ligi Kuu kama Burnley aliyeipandisha Ligi Kuu mwaka 2009, QPR, Blackpool, Watfor, Leeds United na Preston North End, alikumbwa na masaibu hayo asubuhi ya Jumatatu na klabu yake pamoja na vyombo kadhaa vya habari nchini Uingereza vimekuwa vikimtumia na kuandika ujumbe wa kumtakia kila la heri ili apone haraka.
staafu kucheza soka mwishoni mwa msimu wa mwaka  akiwa anaichezea Northampton Town.
Mlinzi huyo wa zamani aliyewahi kuichezea timu ya taifa ya vijana ya Uingereza u21 alitangaza kutundika daluga zake mwishoni mwa msimu uliopita akiwa anaichezea timu ya Northampton Town.
Katika hatua nyingine mke wa mchezaji huyo mstaafu ameishukuru klabu ya Burnley kuonyesha kujali kwa kutangaza kusimama kwa dakika moja kumuombea mumewe apate nafuu.
"Clarke na mimi daima siku zote mioyo yetu ipo Bunrley," Gemma Carlisle aliandika kwenye Twitter.

No comments:

Post a Comment