STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 25, 2014

Gianfranco Zola ateuliwa kuwa kocha mkuu Cagliari

http://metrouk2.files.wordpress.com/2013/09/177634350.jpg
Gianfranco Zola aliyetuliwa kuinoa timu ya Cagliari
NYOTA wa zamani wa kimataifa wa Italia aliyewahi kutamba na timu mbalimbali duniani ikiwamo Chelsea, Gianfranco Zola ameteuliwea kuwa kocha mkuu wa klabu ya Serie A ya Cagliari.
Zola, 48 anachukua nafasi katika timu hiyo baada ya Zdenek Zeman, kutimuliwa mapema wiki hii baada ya Cagliari kuvurunda katika ligi ya Italia na kukamata nafasi ya tatu toka mkiani.
Kocha huyo wa zamani wa West Ham alyeimalizia soka lake katika klabu hiyo ya Cagliari, hakuwa akiinoa timu yoyote tangu alipoachana na Watford mwishoni mwa mwaka jana.
Cagliari imesema mshambuliaji huyo wa zamani wa Azzurri ataanza rasmi kibarua chake siku ya Jumapili kujaindaa na pambano lake la ligi ya Serie A dhidi ya Palermo Januari 6.
Zola, alitumia kipaji chake kuitumikia Chelsea kwa misimu saba kabla ya kugeukia ukocha kwa kuinoa West Ham iliyomfukuza mwaka 2010 kisha kujiunga na klabu ya Watford  aliyokuja kuachana nayo baada ya kujiuzulu katikati ya msimu wake wa pili wa kuinoa klabu hiyo.
Zola anatua Cagliari ikiwa katika hali mbaya kutokana na kushinda mechi mbili tu msimu huu wa ligi kati ya mechi 16 ilizocheza mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment