STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 30, 2014

Spurs yainyoa Everton mabao 2-1

Roberto Soldado
Roberto Soldado scores for SpursTIMU ya Tottenham Hotspur imetakata nyumbani baada ya kuinyoa Everton kwa mabao 2-1 katika pambano kali la Ligi Kuu ya England lililomalizika hivi punde.
Spurs iliyokuwa uwanja wa White Hartlane, ilishtushwa na wenyeji waliotangulia kuandika bao dakika ya 15 kupitia Kevin Mirallas kabla ya Christian Eriksen kusawazisha dakika ya 21 na Saldado aliongeza bao la pili dakika za nyongeza kabla ya mapumziko.
Kwa ushindi huo imeifanya Spurs kufikisha jumla ya pointi 20 sawa na wapinzani wao Arsenal isipokuwa wanakamata nafasi ya saba kwa tofauti na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena siku ya Jumanne kwa mechi sita ambapo Burnley itaikaribisha Newcastle United, Leicester itaialika Liverpool, huku Manchester United ikiikaribisha Stoke City na Swansea City ikiumna ana QPR, wakati Crystal Palace itaumana na Aston Villa na West Brom itapepetana na West Ham.
Jumatano kutapigwa mechi nne, Arsenal dhidi ya Southampton, Chelsea itailika Spurs, Everton itapepetana na Hull City na Sunderland itaialika watetezi Manchester City.

No comments:

Post a Comment