STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 30, 2014

Man City yaipiga Southampton 3-0

Toure skips past the challenge of Southampton midfielder Victor Wanyama in the first half at St Mary's
Yaya Toure akichuana na mchezaji wa Southampton
Midfielder Lampard celebrates his fifth goal for the club with Aguero, after a typical finish from the edge of the box
Wachezaji wa City wakishangilia moja ya mabao yao lililofungwa na Lampard
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City jioni ya leo imepata ushindi mnono wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya 'wagumu' Southampton na kukwea hadi katika nafasi ya pili.
City, hata hivyo ilimaliza pambano hilo ikiwa pungufu kufuatia beki wake Eliaquim Mangala kulimwa kadi nyekundu baada ya kulimwa kadi mbili za njano.
Wageni walianza kuhesabu mabao yake katika dakika ya 51 baada ya kiungo Yaya Toure kuandika bao akimaliza kazi nzuri ya Sergio kun Aguero.
Bao la pili la City liliwekwa kimiania na mkongwe Frank Lampard dakiia ya 80 kabla ya dakika nane baadaye Gael Clichy kumaliza udhia kwa kuandika bao la tatu.
Ushindi huo umeifanya City kupanda hadi nafasi ya pili ikiwa na pointi 27, nane nyuma ya vinara Chelsea na wakiiporomosha Southampton waliokuwa wameng'ang'ania nafasi hiyo kwa muda mrefu ikiwa na pointi zake 26.
City itasafiri siku ya Jumanne kuifuata Sunderland ambayo jana iliikomaliza Chelsea na kutoka nao suluhu.
Ligi hiyo inaendelea tena muda huu kwa pambano jingine linalopigwa Uwanja wa White Hartlane kwa wenyeji Tottenham Hotspur wakiwa mbele kwa mabao 2-1 dhidi ya wageni wao Everton.

No comments:

Post a Comment