STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 30, 2014

AC Milan yaifumua Udinese, Essien alimwa nyekundu

B3sxrK5IUAAcGQY Michael Essiens epic reaction to sending off during AC Milan v Udinese [video]
Michael Essien akiwa haamini kama kalimwa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi ya pili ya njano
Italy Soccer Serie A
Jeremy Menez akifunga bao la Ac Milan
 MABAO mawili yaliyowekwa kimiani na Jeremy Menez, moja likiwa na mkwaju wa penati yametosha kuipa ushindi timu ya AC Milan katika pambano la Ligi Kuu ya Italia 'Serie A' dhidi ya Udinese.
Milan ikiwa nyumbani hata hivyo kama ilivyokuwa kwa wageni wao, walijikuta wakipoteza mchezaji mmoja baadaya Michael Essien kulimwa kadi mbili za njano, dakika chache tangu Udinese wampoteze Domizzi kwa rafu aliyomchezea Kaisuyke Honda na kusababisha penati ilifungwa na Menez katika dakika ya 65.
Menez aliongeza bao la pili dakikia 10 baadaye akimalizia kazi nzuri ya Boneventura na kuifanya AC Milan kukwea hadi nafasi ya tano ikiwa na pointi 21.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo, Cagliari ikiwa nyumbani ilijikuta ikifumuliwa mabao 4-0 na Fiorentina nayo Cesena pia ililala nyumbani kwa mabao 3-0 na genoa huku Empoli na Atalanta zilitoshana nguvu kwa kutofungana na Palermo ikitakata nyumbani kwa kushinda mabao 2-1 dhidi ya Parma na hivi sasa watetezi Juventus wapo nyumbani ikiumana na Torino na mpaka sasa ikiwa ni mapumziko matokeo ni 1-1.

No comments:

Post a Comment