STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 14, 2014

Walcott aleta faraja Emirates, arejea dimbani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7rsOPqad07I0-k-H9Wizxmhn3SadOqRP-R8t_WrVlo9OuD_iKPU-5OrSvwOjl7ep-fECxEgRe76HGH3E813ae1BNR-w-C9Q2n7-kgAj7OJ9wvRHEa9Jqllo3WVvlDEy7ddyizp79fZBea/s1600/Theo+Walcott+wallpaper+13.jpgWINGA machachari, aliye nyota wa Uingereza, Theo Walcott ameleta faraja kwa mashabiki wa Arsenal baada ya kurejea dimbani kutoka kwenye hali ya majeruhi kwa muda wa miezi 10 iliyopita kwa kujiumiza vibaya goti lake.
Walcott, 25, hajacheza tangu kukata mishipa ya goti lake la kushoto kwenye ushindi wao wa 2-0 dhidi ya wapinzani wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspurs katika Kombe la FA Januari.
“Ni shangwe kukukaribisha tena @theowalcott!” Arsenal waliandika kwenye anwani yao rasmi ya mtandao wa kijamii wa Twitter pamoja na picha yake akipasha misuli na wenzake.
Arsenal watakaribisha Hull City Jumamosi kwenye pambano la Ligi Kuu ya England akiungana na kiungo mwenzake wa pembeni, Serge Gnabry aliyekuwa akiuguza pia goti tangu Machi.
Wawili hao wameinua mioyo ya Ze Gunnerz ambayo itawakosa nyota wake kadhaa waliopo kwenye 'wadi' ya majeruhi viunga vya Emirates akiwamo Mesut Ozil.

No comments:

Post a Comment