STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 14, 2014

Argentina yaiangamiza Hong Kong, Messi aanzia benchi

International friendlies - Argentina stroll to seven-goal victory over Hong Kong
Wachezaji wa Argentina wakipongeza kwa kuinyoa Hong Kong mabao 7-0
ARGENTINA iliyotoka kukung'utwa mabao 2-0 na Brazil mwishoni mwa wiki nchini China, leo imezinduka kwenye mechi zake za kirafiki za kimataifa baada ya kuinyoa Hong Kong mabao 7-0.
Ever Banega alianza kuiandika wageni bao dakika ya 19 kabla Gonzalo Higuan kuongeza la pili katika dakika 42 kwa pasi ya Vangioni na Nicolas Gaitan kuongeza la tatu sekunde chache kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili Higuan alikianza kwa kuongeza bao la tatu dakika ya 54 akimalizia kazi ya Gaitan na baada ya Messi kuingia dimbani aliongeza bao la tano dakika ya 66 kwa kazi nzuri ya Banega.
Gaitan hakutosheka kwa kufunga bao jingine lililokuwa la sita kwa Wanafainali hao wa Kombe la Dunia kwenye dakika ya 72 na Messi kuongeza bao la mwisho  dakika sita kabla a filimbi ya mwisho.

No comments:

Post a Comment