STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 4, 2011

Wasanii wa kike tujiheshimu-Regina



MMOJA wa waigizaji wa filamu anayekuja juu nchini, Regina Mroni amewaasa wasanii wenzake hususani wa kike, kujiheshimu na kuepukana kufanya matendo yanayowachafua mbele ya jamii pamoja na kuidhalilisha fani yao kuonekana kama kazi ya wahuni.
Mroni, aliyeng'ara kwenye filamu kama Trip to Amerika, Mastress, Siri y Mama, Aisha na nyinginezo, alisema kuna baadhi ya wasanii hasa wa kike wamekuwa wakiona raha kujianika utupu na kuhusishwa na skendo chafu, wakiamini wanakuza majina yao wakati wanajidhalilisha.
Alisema umaarufu wa msanii yeyote unapatikana kutokana na ubora na umahiri wa kazi zake na sio matendo machafu na hivyo kuwataka wasanii wa kike wajiamini, kujituma na kuithamini kazi yao ili jamii iwaheshimu.
"Wapo baadhi yetu wamekuwa wakijihusisha na matendo machafu na kuandikwa kila mara, kitu ambacho tofauti na fikra zao kuwa wanajijengea majina na umaarufu, wanajidhalilisha na kuonekana mbele ya jamii kama watu wasio na maadili kitu ambachio ni kibaya," alisema Mroni.
Mroni, aliyetumbukia kwenye fani hiyo miaka miwili iliyopita akitokea kwenye urembo ambapo aliwahi Miss Utalii Morogoro, Miss Ukonga, Miss Singida na kushiriki Miss Tanzania, alisema sanaa ni kazi kama kazi nyingine na wanaishiriki waithamini na kuipenda.
Alisema 'wavamizi' wachache kwenye fani hiyo wasio na vipaji ndio wanaojiachia na kujianika na mwisho wa siku wanadhalilika na kisha kupotea wakiwaacha wasanii wa kweli wakiendelea kutamba.

Mwisho

No comments:

Post a Comment